Wednesday, October 15, 2014

Kutoka kushoto Saimon Msuva Geilson Santos Santana 'Jaja' na Mrisho Ngassa

KOCHA mkuu wa Yanga, Mbrazil, Marcio Maximo amekazania kuwafundisha wachezaji wake namna ya kumiliki mpira, kupiga pasi za uhakika, kushambulia kwa kasi na kujilinda vizuri kuelekea katika mechi ya watani wa jadi ya ligi kuu soka Tanzania bara dhidi ya Simba sc itakayopigwa Oktoba 18 mwaka huu uwanja wa Taifa, Dar es salaam.

Maximo ambaye anakinoa kikosi chake katika uwanja wa Boko Veterani uliopo nje kidogo ya jiji la Dar es salaam  amejikita zaidi kuwaandaa mawinga wake hatari, Mrisho Khalfan Ngassa ‘Anko’ na Saimon Happygod Msuva ili kuwaua mahasimu wao wanaonolewa na kocha Mzambia, Patrick Phiri.

Mbrazil huyu mwenye heshima kubwa hapa nchini imeonekana kuwaandaa Ngassa na Msuva kwa muda mrefu, na hii inamaanisha atashambulia zaidi akitumia mawinga wa pembeni wenye kasi kubwa.

Ngassa na Msuva kwa muda mrefu wamekuwa wakifundishwa kupiga krosi kali zenye madhara langoni, huku nao Nizar Khalfan, Hussein Javu na Andrey Coutinho wakifundishwa zoezi hilo kwa muda mrefu.


Wakati Yanga wakiwa Dar, Simba wao wapo bondeni‘Sauzi Afrika’ wakinoa makali yao.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video