Saturday, October 4, 2014

Ijapokuwa wapo uwanja wa nyumbni( Mabatini),lakini bado Ruvu Shooting wana hali ngumu zaidi kuelekea katika mchezo wa leo Sep 4, 2014 dhidi  ya wagonga nyundo kutoka Mbeya, Mbeya City Fc kutokana na mahesabu ya wazi kuelekea katika mchezo huo wa tatu tangu msimu mpya 2014/2015 ya ligi kuu Vodacom Tanzania Bara ianze.
Kwa sasa Ruvu Shooting wanaburuza mkia katika msimamo wa ligi ya VPL 2014/2015 wakiwa wamepoteza michezo yote miwili ya awali na hawana pointi yoyote.
Ruvu Shooting chini ya  mwalimu mkuu, Tom Alex Olaba, walikubali kupoteza jumla ya michezo miwili mfululizo tena wakiwa uwanja wa nyumbani. Mchezo wa kwanza wa ufunguzi walijikuta wakichezea kipigo cha magoli 3-0 kutoka kwa bingwa mtetezi wa ligi kuu Tanzania Bara, Azam Fc, na kama hiyo haitoshi bado wakaruhusu kufungwa magoli 2-0 kutoka kwa wajelajela, Tanzania Prisons ya Mbeya.

Kwa matokeo hayo ya awali, hakuna ubishi kwamba, Ruvu shooting msimu huu hawana wachezaji wazuri, na kama wana wachezaji wazuri basi, benji la ufundi halijafanikiwa kuteua wachezaji wenye uwezo kwa ajili kushindana kupata ushindi. Mpaka sasa ni vigumu kusema Ruvu shooting wana nafuu katika idara gani kwani hawaezi kufunga magoli, lakini pia wanaruhusu magoli mengi.

Akilonga na mtandao huu, msemaji wa Ruvu Shooting, Masau Bwire ( Bwana Mipasho) alisema wamechoshwa na matokeo duni ya mechi za awali za ufungizi wa ligi tena katika uwanja wa nyumbani.

"Ndugu yangu, nachoweza kusema ni kwamba sisi Ruvu Shooting hatuja pendezwa na matokeo ya mechi mbili zilizopita ambazo tulipoteza. Lakini, tumetambua matatizo yetu na kikosi chetu chini ya kocha bora, Tom Olaba kimeanza kufanya marekebisho muhimu ili kuhakikisha tunapata matokeo mazuri katika mechi yetu dhidi ya Mbeya City siku ya Jumamosi". Masau alisema.

Lakini kwa upande wake kocha mkuu wa Mbeya City FC, Juma Mwambusi, amesema mechi ya leo dhidi ya Ruvu Shooting ni mchezo muhimu sana kwao kwa  kuwa ni mchezo wa kwanza wakiwa ugenini msimu huu  na wangependa kupata ushindi ili kuendelea kujiweka vizuri katika msimu wa ligi.

Hata hivyo nao, Mbeya City Fc hawako katika kiwango cha kusisimua kama ilivyokuwa msimu wa jana, kwani kati ya michezo miwili ambayo wamekwisha cheza, wametoka suluhu na Ruvu Stars na kushinda goli 1-0 dhidi ya Costal Union tena kwa mbinde.

Huu utakuwa ni mchezo wa kukamia zaidi leo katika dimba la Mabatini, kwani Ruvu Shooting watataka kurudisha imani kwa mashibiki wake, lakini nao Mbeya City watataka kulinda sifa yao nzuri ya kuwa timu chipukizi bora ya msimu uliopita.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video