Friday, October 10, 2014

MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Togo, Emmanuel Adebayor yuko safarini kwenda Kampala tayari kwa mechi ya wiki hii ya kuwania kufuzu fainali za mataifa ya Afrika, Afcon 2015 dhidi ya Uganda The Cranes.

Siku chache zilizopita Adebayor hukuwepo kwenye kikosi cha Togo wakati wa mazoezi mjini Lome na hali hii ilizua wasiwasi kwamba angekosa mechi hiyo muhimu.

Hata hivyo, Supersport.com imethibitisha kuwa nyota huyo anayekipiga klabu ya Tottenham inayoshiriki ligi kuu soka nchini England amekuwepo Uganda asubuhi ya leo akitokea Nairobi.

Togo haina pointi yoyote kufuatia kupigwa 2-1 na Guinea mjini Casablanca na 3-2 kutoka kwa Ghana katika uwanja wao wa nyumbani.


Mechi dhidi ya Uganda ndio itatoa picha halisi ya nani ana nafasi kubwa ya kufuzu katika mashindano hayo yakayofanyika nchini Morocoo.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video