Monday, September 15, 2014

BAADA ya kuinyuka Mbeya City fc mabao 4-1 katika uwanja wa Sokoine jijni Mbeya mwishoni mwa wiki iliyopita, Vipers FC (zamani Bunamwaya) inayoshiriki ligi kuu nchini Uganda, itashuka dimbani kucheza mechi nyingine ya kirafiki dhidi ya Ruvu Shooting ya mkoani Pwani .

Mechi hiyo itapigwa kesho (septemba 16 mwaka hu) uwanja wa Taifa, Dar es salaam.

Afisa habari wa Ruvu Shooting, Masau Bwire amesema kikosi cha Shooting chini ya kocha Mkenya, Tom Alex Olaba kimejiandaa vizuri, hivyo mashabiki wa soka wajitokeze kuiona timu mpya yenye makazi yake Mabatini, Mlandizi, Pwani.


“Kesho katika uwanja wa Taifa tutakuwa na mchezo maridadi wa kirafiki wa kimataifa. Tutacheza na timu ya Vipers FC ya Uganda iliyotoka kutoa kipigo cha haja kwa ndugu zetu Mbeya City”.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video