Monday, September 29, 2014

Maximo (kushoto) alifurahia ushindi wa 2-1 dhidi ya Prisons jana uwanja wa Taifa

Na Baraka Mpenja, Dar es salaam



KOCHA mkuu wa Yanga, Mbrazil, Marcio Maximo kwa mara ya pili alikutana na kocha Mzawa katika michuano ya ligi kuu soka Tanzania bara.

Ikitokea nchi ya mbali (Brazil) ambayo hunukia harufu ya soka kila kona, Maximo alitandikwa 2-0 uwanja wa Jamhuri, Morogoro na Mtoto wa Kitanzania, Mecky Mexime , kocha wa Mtibwa Sugar.

Jana akakutana na Mtanzania mwingine, David Mwamwaja, kocha wa Tanzania Prisons na kufanikiwa kushinda 2-1.

Katika mechi zote hizo mbili, maarifa ya Maximo yalionekana kuelekeana na pengine kuzidiwa kwa kiasi kikubwa na ya wazawa.

Kama Prisons wangekuwa makini safu ya ushambuliaji na kuongeza nidhamu ya ulinzi, dhahiri walikuwa wanamharibia siku Maximo.

Lakini kocha huyu aliyewahi kuifundisha timu ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars, kati ya 2006 na 2010 ameendelea kuzungumza mpira na sio unazi kila baada ya mechi.

Hajisifu hata kidogo, pale anapokosea anakiri waziwazi na kuahidi kujipanga zaidi.

Alipofungwa Morogoro aliwasifu Mtibwa kwa kucheza vizuri, akaisifu timu yake kwa kucheza vizuri ingawa ilifanya makosa sehemu ya ushambuliaji na safu ya ulinzi.

Alisema hakuna haja ya kukata tamaa, mpira ndivyo ulivyo, ligi ndio inaanza, lakini akaahidi kuwa mechi ijayo (ya jana dhidi ya Prisons) timu itaimarika zaidi.

Katika mechi hiyo, Yanga walionesha kubadilika, lakini safu ya ulinzi iliendelea kuwa na makosa mengi.

Lakini Maximo hajakata tamaa, anajiona kuwa ana nafasi ya kuboresha zaidi eneo hilo.

Baada ya mechi, Mtandao huu uliinasa kauli ya Maximo kwa umakini kabisa akisema: “Lakini tunatakiwa kukaa chini na kujiboresha kiukweli, wachezaji wanakuja-kuja, baada ya wiki moja watakuwa wazuri zaidi. Tuna wiki moja ya maandalizi kabla ya mechi, tutafanya mazoezi zaidi na tutakuwa imara zaidi mechi ijayo”.

Kwa upande wa Kocha wa Prisons, David Mwamwaja, hali ilikuwa tofauti. Alimlalamikia mwamuzi, Andrew Shamba akidai aliipa mbeleko Yanga.

Mwamwaja alisema: “Kiujumla vijana walijituma na kuonesha uwezo mkubwa wakiwa wachache. Nina masikitiko kwasababu waamuzi hawakunitendea haki. Wale wachezaji wa Yanga walishika mpira mara tatu ndani ya penalti boksi, lakini hawakupewa adhabu yoyote”

“Hii mechi ingekuwa tofauti kama wangetoa haki. Mimi najali uwezo wa vijana. Mchezaji wangu alioneshwa kadi nyekundu (Jacob Mwalobo), lakini ilikuwa sio. Tutajitahidi zaidi mechi ijayo”.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video