Monday, September 29, 2014

Fred Minziro ( mbele kulia) akitoka uwanjani kwenye moja ya mechi za ligi kuu uwanja wa Taifa msimu uliopita

Na Baraka Mpenja, Dar es salaam



JKT Ruvu chini ya kocha wa zamani wa Yanga, Fred Felix Minziro iliambulia kichapo cha 2-0 kutoka kwa Kagera Sugar katika mechi ya raundi ya pili ya ligi kuu soka Tanzania bara iliyopigwa uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es salaam.

Mabao ya Kagera yalifungwa na Salum Kanoni katika dakika ya 10 na Rashid Mandawa dakika ya 79.

Huo ulikuwa ushindi wa kwanza kwa Kagera msimu huu kufuatia kipigo cha 1-0 dhidi ya Mgambo JKT katika mechi ya ufunguzi uwanja wa CCM Mkwakwani Tanga.

JKT Ruvu wao wanapoteza mechi ya kwanza nyumbani kufuatia kutoka 0-0 na Mbeya City ugenini wikiendi ya septemba 20 mwaka huu.

Maafande hao jana hawakucheza vizuri ukilinganisha na mechi ya kwanza kule Mbeya, hivyo ilikuwa halali kuchapwa na Wakata miwa wa Kaitaba.

Kocha Minziro alikiri wazi kuwa kikosi chake hakikufanya kazi nzuri, lakini wana takribani wiki moja ya kujiandaa kabla ya mechi dhidi ya Yanga.

Minziro alisema: “Kwakweli nimeyapokea kwa masikitiko makubwa matokeo haya. Hali haikuwa nzuri kwa upande wangu. Tulipoteza umakini na tuliwapa nafasi rahisi wapinzani wetu na wakapata magoli”


“Tumefanya makosa ya kimchezo, nadhani tutafanyia kazi kabla ya mechi dhidi ya Young Africans”.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video