Saturday, September 27, 2014

Na Baraka Mpenja, Dar es salaam

0712461976

SIMBA SC inawakosa wachezaji wanne muhimu katika mechi yake ya pili, ligi kuu soka Tanzania bara inayopigwa leo jioni dimba la Taifa, Dar es salaam dhidi ya Maafande wa Polisi Morogoro.

Wachezaji hao ambao kocha Patrick Phiri atawakosa ni kipa namba moja, Ivo Philip Mapunda, beki wa kushoto, Issa Rashid ‘Baba Ubaya’, Winga hatari Haroun Chanongo na Mshambuliaji Paul Kiongera , wote ni majeruhi.

Mechi ya ufunguzi wikiendi iliyopita ambayo Simba ililazimishwa sare ya 2-2 na Wagosi wa Kaya, Coastal Union katika uwanja huo wa Taifa, Issa Rashid pekee ndiye hakucheza kati ya wachezaji hao wanne.

Ivo alisimama langoni na alifanya jitihada kubwa kuisaidia timu yake ipate ushindi, lakini hakufanikiwa kufuatia kuruhusu nyavu zake kuguswa mara mbili.

Licha ya kufungwa, Ivo hakustahili lawama za moja kwa moja, kwasababu magoli yote mawili yalitokana na timu kushindwa kudhibiti eneo la kiungo na kuwaacha Coastal wafike golini na kutengeneza nafasi za mabao.

Makosa binafsi ya beki kinda, Hassan Isihaka yalichangia Simba kufungwa, lakini kijana huyu mdogo aliyerithi mikoba ya Donald Mosoti hakustahili lawama kwasababu ndio kwanza anachipukia.

Chanongo alicheza dhidi ya Coastal Union lakini aliumia. Mshambulijai huyu wa pembeni katika mechi hiyo hakucheza kwa kiwango chake.

Hakutumia staili yake ya kukimbia na mpira, kupunguza mabeki na kuingia ndani. Mipira mingi aliyoshika katika eneo la hatari alikuwa anageuka na kutoa pasi.

Chanongo alionekana kuwa muoga kuwafuata mabeki kama alivyokuwa anafanya msimu uliopita. Inawezekana hayuko sawa kisaikolojia kutokana na kuwahi kushutumiwa kuuza mechi.

Kiongera alitokea benchi, lakini alipata majeruhi katika dakika za majeruhi. ‘Baba Ubaya’ hakucheza kabisa na nafasi yake ilishikwa na Mohammed Hussein ‘Tshabalala’.

Paul Kiongera hachezi leo

Kutokana na usajili mzuri waliofanya Simba, Kipa bora wa msimu uliopita, Hussein Sharrif ‘Casillas’ ataziba nafasi ya Ivo, Ibrahim Twaha anaweza kuchukua nafasi ya Chonongo, nafasi ya Issa bado ataendelea kucheza Tshabalala wakati nafasi ya Kiongera anaweza kuziba na Elias Maguli.

Mechi iliyopita, Simba walianzia kufa katikati. Piere Kwizera aliyecheza nafasi ya kiungo wa ulinzi alishindwa kupiga pasi katika maeneo sahihi.

Kwa kiasi kikubwa alikuwa anapiga pasi sahihi, lakini hazikuwa na madhara. Kuna wakati alikuwa anachelewa kuanzisha ‘Movement’ kwa kwenda mbele.

Kama atabadilika leo na kuipandisha timu kwenda mbele, basi Simba inaweza kufanya vizuri. Pia itakuwa nzuri kama Phiri atamuanzisha Shaaban Kisiga nafasi ya kiungo mshambuliaji (namba 10).

Kisiga huwa anacheza kwa ubora wa hali ya juu katika nafasi hiyo. Huwa anaweza kupiga pasi nzuri na kuipandisha timu kwa kasi, lakini kitendo cha kuchezeshwa namba 8, kinamfanya asitoe ubora wake.

Kwa safu ya ushambuliaji, nadhani Amissi Tambwe ataendelea kuwa mtu hatari. Lakini itategemea na viungo wake na watu watakaokuwa nyuma yake.

Sitegemei kuona maajabu kutoka kwa Emmanuel Okwi kama atakuwepo. Mpaka leo asubuhi hakukuwa na taarifa za nyota huyo kupewa kibali cha kufanya kazi nchini licha ya kusajiliwa kihalali na Simba.

Okwi amepunguza kasi yake, haingia ndani kama zamani, nadhani imechangiwa na kutocheza mpira wa muda mrefu. Ni mchezaji hatari, lakini kwasaa dhahiri anahitaji kupewa muda na kufanya mazoezi maalumu ili kurudisha kasi yake.

Emmanuel Okwi (kulia)

Tambwe ataendelea kuwa mtu muhimu na kama atapigiwa mipira ya krosi na pasi nyingi za mwisho, basi anaweza kufunga.

Simba wanaweza kuvuna pointi mbele ya Polisi Morogoro, lakini sio kwa kirahisi tu. Mshambuliaji wa zamani wa Simba na Taifa Stars, Danny Mrwanda ni mchezaji wa kuchungwa sana.

Mwaka juzi alisajiliwa na Simba, lakini alitemwa kabla ya kuanza ligi kwa madai kuwa ameshuka kiwango na baadaye akatimkia Vietnam.

Aina ya mchezaji kama Mrwanda ni hatari sana, na kwakuwa Simba walishindwa kuona thamani yake, anaweza kuingia uwanjani kwa lengo la kutaka kulipa kisasi.

Kama Bantu Admin na Suleiman Kassim ‘Selembe ‘ watakuwa katika ubora wao na kumlisha mipira sahihi, nadhani Mrwanda  anaweza kufanya kitu.

Nahodha wa Polisi, Lulanga Mapunda ni mtu sahihi sehemu ya ulinzi. Ni mzoefu sana, hivyo imekuwa rahisi kwake kuwa kiongozi uwanjani.

Kwenye mechi dhidi ya Azam, Polisi walifungwa 3-1. Na kipindi cha kwanza walionekana kuwa na hofu kubwa, walitawaliwa na Azam kwa kila kitu.

Waliruhusu mpira kucheza zaidi katika eneo lao, hivyo vijana wa Joseph Omog waliweza kupanga mashambulizi mengi. Kama washambuliaji wa Azam, Kipre Tchetche, Didier Kavumbagu wangekuwa makini, basi wangefunga magoli mengi.

Lakini kipindi cha pili walibadilika na kujaribu kucheza mpira. Bila shaka kocha Adolf Rishard aliona makosa yake na kuyafanyia kazi.

Polisi hawana rekodi ya kushinda dhidi ya Simba uwanja wa Taifa, kama Historia haitawatendea haki, basi wataendelea kufungwa.


Lakini Simba wasiingie kichwa-kichwa, mpira umebilika siku hizi. Timu ndogo inaweza kupata matokeo pia.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video