Monday, September 15, 2014

Kikosi cha Ndanda fc kilichotoka suluhu dhidi ya Simba sc jumamosi iliyopita uwanja wa Nangwanda Sijaona, Mkoani Mtwara.

Na Baraka Mpenja, Dar es salaam
KUCHEZA mechi ya kirafiki dhidi ya Simba wikiendi iliyopita kumewafanya Ndanda fc wabaini kasoro za kikosi chao kabla ya kuanza kwa ligi kuu Septemba 20 mwaka huu.

Ndanda fc waliopanda ligi kuu msimu huu wataanza kampeni zao dhidi ya wageni wenzao wa Stand United katika uwanja wa Kambarage mjini Shinyanga, septemba 20 mwaka huu.

Kocha mkuu wa klabu hiyo, Denis Kitambi  amesema mechi dhidi ya Simba iliyomalizika kwa suluhu pacha ya bila kufungana (0-0) katika uwanja wa Nagwanda Sijaona jumamosi iliyopita imewafanya waweze kubaini makosa yao hasusani safu ya ushambuliaji.

“Tulifuraki kupata mechi na timu kubwa yenye ushindani mkubwa. Kiufundi kuna mambo kadhaa tumeyabaini. Kwanza kabisa tunashindwa kutumia nafasi ambazo tunatengeneza, kwahiyo inabidi tulifanyie kazi.”

“Pia kuna matatizo katika uanzishaji wa mpira kutoka nyuma, nalo  tunatakiwa tulifanyie kazi.”

“Simba ina ufundi mwingi, kwahiyo ilikuwa mechi muhimu kwasababu watu kama hao tutacheza nao katika ligi. Tutacheza na Simba, Yanga , Azam ambao kiufundi unatakiwa kujiandaa zaidi kuliko ule ufundi binafsi wa wachezaji”

“Mimi naamini wachezaji tulionao hatuwezi kuongeza wa ziada wala kuwapa lawama sana, kwasababu jambo la kupanga mashambulizi tunaanza kulifanyia kazi wiki hii iliyobaki na tunataka kucheza kitimu na kupata magoli.”

“Pia nawapa pongezi wachezaji wangu kwasababu wanaweza kutengeneza nafasi, hii ilionekana katika mchezo na Simba na mechi nyingine za nyuma, lakini bado tunahitaji kuzitumia hizo nafasi”.

Kuhusu mechi ya ufunguzi wa ligi kuu dhidi ya Stand United, Kitambi alisema atapata changamoto kubwa kutokana na mazingira ya ugenini.

“Mechi hiyo kwa kiasi fulani imelemea upande wa Stand United kwasababu wapo nyumbani na unajua wote tumepanda daraja, kwahiyo na sisi wenyewe tunajua hapo ndipo tunaweza kupata pointi na wenyewe wanajua  wanaweza kupata pointi kwetu”


“Faida kwao ni kwamba watacheza nyumbani, kwahiyo mechi hii itakuwa na changamoto kubwa ukizingatia usafiri kutoka huku Mtwara kwenda Shinyanga na utatuchosha”

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video