Friday, September 26, 2014

Edo akishangilia moja ya goli alilofunga akichezea Simba sc

Na Baraka Mbolembole

Akitokea benchi, mshambulizi Edward Christopher aliisaidia Simba SC kuibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Ruvu Shooting. Ilikuwa ni  Septemba 24 wakati kocha Milovan Circovic alipomuingiza uwanjani kijana wa miaka 20 ( wakati huo).

 Christopher alikuwa ametoka kushinda tuzo binafsi ya ufungaji bora katika michuano ya ABC Super8, mwezi mmoja nyuma huku akiisaidia klabu yake kutwaa ubingwa huo kwa kuilaza Mtibwa Sugar kwa mabao 5-3 katika fainali ambayo kabla ya mechi mchezaji huyo alimuahidi  golikipa Shaaban Kado wa Mtibwa kuwa atamfunga ‘ hat-trick’, na kweli akafanya hivyo.

Mara baada ya michuano hiyo Christopher alitabiriwa kama mmoja wa wachezaji bora vijana nchini Tanzania ambao watafanya mambo makubwa. Ilikuwa ni ndoto iliyotimia kwa mchezaji huyo kupangwa katika kikosi cha kwanza cha Simba katika pambano dhidi ya mahasimu wao Yanga SC, Jumatano ya Oktoba 3, 2012 katika mchezo wa ligi kuu Tanzania Bara msimu wa 2012/13.

Akiwa kinda wa miaka 20, Milovan alikunwa na kipaji cha kukotota mpira cha mchezaji huyo, umaliziaji wake wa kiwango cha juu na namna alivyo na maarifa ya kupasua ngome za timu pinzani.

Mbele ya mashabiki ‘ lukuki’ katika uwanja wa Taifa, Simba na Yanga zilicheza kandanda safi. Amri Kiemba alifunga bao safi la mkwaju wa mbali nje kidogo ya eneo la mita 18 akiunganisha moja kwa moja krosi iliyopigwa na Mwinyi Kazimoto kutoka wingi ya kulia.

Said Bahanunzi alikuja kufunga bao la kusawazisha kwa mkwaju wa penalti mwishoni wa kipindi cha pili na kutengeneza sare ya kufunga bao 1-1. Ilikuwa ni moja ya mechi zilizojaza watazamaji wengi katika uwanja huo, huku timu zote zikicheza soka la kushambulia na nguvu.

Yanga walikuwa wametoka kufungwa mabao 5-0 katika mchezo wa mwisho wa ligi kuu, iliingia kucheza na Simba ikiwa na ubingwa wa Kagame Cup, huku usajili wao wa mlinzi Mbuyu Twite ukiwa mchungu kwa Simba.

 Ilikuwa mechi ya Christopher,  alimsumbua vilivyo mchezaji huyo wa Kimataifa wa Rwanda. Edo alikuwa akitokea pembeni ya uwanja upande wa kushoto jukumu ambalo lilimfanya kuwa tishio kwa Mbuyu kila alipokuwa na mpira.

Mbuyu alimpiga sana viatu kijana huyo ambaye alivumilia na kuendelea kuwasumbua walinzi wa Yanga na kuwa tishio langoni mwao. Kasi ya kijana huyo ilikuwa juu mno na kufanya Simba kushambulia muda wote ambao alikuwepo uwanjani kabla ya kuumizwa na Mbuyu.

Mchezaji huo aliuguza majeraha yake lakini kila aliporudi uwanjani aliendelea kusumbuliwa na maumivu. Simba ilimvumilia kwa muda wote na kufikiri kuwa mchezaji ataimarika na kurejesha kiwango chake lakini aliishia kugombana na Walimu, Jamhuri Kiwelo na Abdallah King Kibadeni msimu uliopita, hata alipokuja  Zdravko Logarusic bado mchezaji huyo alitajwa kama mmoja wa wachezaji ambao wanacheza kwa viwango vya chini katika timu hiyo. Alirudishwa benchi na Loga na baadaye mwalimu huyo raia wa Croatia alipendekeza mchezaji huyo aachwe.

Christipher aligoma kuuzwa kwa mkataba wa mkopo hivyo alikwenda katika timu ya Mtibwa Sugar kujifua wakati akisikilizia ni wapi hasa anaweza kucheza na kuendeleza kipaji chake. Mwalimu Adolf Richard alimsaini mchezaji huyo kwa mkataba wa mwaka mmoja katika kikosi cha Polisi Morogoro.

 Ikiwa tayari imepoteza mchezo wa kwanza mbele ya Azam FC wiki iliyopita, Polisi itacheza mchezo wa pili mfululizo ikiwa katika jiji la Dar es Salaam, na Jumamosi hii watacheza na moja ya timu yenye uhasama nayo kwa muda mrefu ndani ya uwanja.

Polisi imekuwa ‘ nyanya’ katika uwanja wa Taifa mbele ya Simba lakini mabingwa hao mara 19 wa kihistoria wamekuwa na wakati mgumu kila wanapotua katika uwanja wa Jamhuri, Morogoro.

 Ukitoa uwepo wa Christopher, Adolf atakuwa na wachezaji wengi wa kujivunia katika mchezo huo kama nahodha, Nahoda Bakari, Lulanga Mapunda, Danny Mrwanda na nyota wengine wengi.  Simba SC v Polisi Morogoro hii ni nafasi pekee ya ‘ Edo Boy’ kuwakumbusha watu kuhusu kipaji chake akiwa na miaka 22 hivi sasa.

Je, Christopher atafunga katika mchezo wa kesho?. Inawezekana kwa sababu tayari safu ya ulinzi ya Simba imeruhusu mabao mawili katika mchezo wa kwanza, huku Polisi wakiwa tayari wamefunga bao moja katika uwanja wa Azam Complex Chamanzi. Simba watamchunga sana Christopher sababu wanamfahamu lakini atawafunga wakijisahau kidogo tu.


0714 08 43 08

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video