Monday, September 15, 2014

Geilson Santos Santana 'Jaja' (katikati) akishangilia bao lake na Mrisho Ngassa (kulia) na Saimon Msuva (kushoto)

Na Baraka Mpenja, Dar es salaam
0712461976

KAZI ya kwanza ya mshambuliaji uwanjani ni kufunga magoli, ingawa anaweza kusaidia mambo mengine kama kurudi kusaidia timu pale inaposhambuliwa, kutoa pasi kwa wenzake na mambo mengine ya kimpira.

Mchezaji anapopewa majukumu ya kuwa mshambuliaji wa mwisho, hesabu zake lazima zijikite kutafuta nyavu na hapo ndipo atawafurahisha makocha wake, wachezaji wenzake, viongozi wa timu na hatimaye mashabiki.

Kuna washambuliaji wa aina nyingi duniani na kamwe hawawezi kufafana kwa aina ya uchezaji wao. Lionel Messi hafanani uchezaji wake na Cristiano Ronaldo. Karim Benzema hafafani uchezaji wake na Diego Costa, lakini wote wanaweza kufunga kadri wawezavyo.

Kufunga ni kufunga tu. Unaweza kupiga kichwa, shuti au kufungia tumbo na likawa goli. Sio lazima kila mshambuliaji afunge kwa ‘staili’ ya Cristiano Ronaldo ya kupiga mashuti.

Baadhi ya mashabiki wa soka wamekariri vitu fulani, kila muda wanataka kumuona kila mshambuliaji ana kasi, chenga na shabaha ya kuona lango, kumbe sio lazima iwe hivyo.

Thomas Ulimwengu ana uwezo mkubwa wa kuwasumbua mabeki kwa ‘manguvu’ yake na akafunga. Ni aina ya wachezaji wenye uwezo wa kutumia nguvu na kupambana kwa mabavu, lakini hana vitu vingi kama kupiga chenga au kimtaa zaidi ‘kupaka rangi mpira’.

Uchezaji wa Ulimwengu ni tofauti na  Mbwana Samatta. Wote wanaweza kufunga, lakini Samatta ana vitu vingi, anaweza kuchezea mpira, kukimbia nao kwa kasi, kupiga chenga akitokea pembeni na hata katikati.

Leo hii huwezi kutaka Samatta acheze kama John Bocco. Hawa ni watu wawili tofauti na ndio maana mmoja ni Samatta na mwingine ni Bocco. Kiuchezaji wanatofautiana kabisa, lakini wote wanaweza kufunga.

Naweza jamani!: Jaja akishangilia moja ya bao lake

Mashabiki wa soka la Tanzania wanabadilika-badilika sana. Leo wanaweza  kukuzomea, kesho wakakushangilia kama mfalme.
Siku ya kwanza kwa Geilson Santos Santana ‘Jaja’  kuonekana uwanja wa Taifa ilikuwa katika mechi ya kimataifa ya kirafiki  kati ya Yanga na Thika United ya Kenya.

Jaja alifunga bao pekee katika ushindi wa 1-0, lakini hakukubalika kwa mashabiki waliofika uwanjani hapo wakidai ni mzito sana.

Pamoja na uzito wake, aliwafungia bao la ushindi. Kabla ya bao hilo, Jaja alifunga bao katika mechi ya kirafiki dhidi ya Chipukizi uwanja wa Gombani, Pemba.

Jaja alikejeliwa sana na pengine kutokujua Kiswahili kumemsaidia na hata kama aliambiwa na mtu yeyote, bado asingeweza kushangaa kwasababu mpira ni kazi yake na amezoea presha ya mashabiki.

Imani yangu ni kubwa kwa kocha Marcio Maximo. Najua alimleta Jaja kwa kazi moja tu ya kufunga mabao.

Maximo ni mwalimu mwenye msimamo na afanyapo jambo huwa anajua sababu. Alishawahi kusema Jaja ni mfungaji mzuri ‘Goal Machine’, hivyo apewe muda.

Kocha huyu raia wa Brazil anajua fika kuwa Jaja sio mtu wa vitu vingi, hajui kuchezea mpira, hana kasi kubwa, yaani anacheza ‘kivivu’, lakini amejaaliwa kitu cha msingi sana kama mshambuliaji.

Jaja (wa pili kulia, waliosimama wima) alifunga mabao mawili katika ushindi 3-0 dhidi ya Azam fc

Anajua kukaa kwenye nafasi na kuliona goli. Jana dhidi ya Azam fc alianza  ‘Mdogo mdogo’. Kipindi kizima cha kwanza hakuonekana kabisa zaidi ya kuwaona akina Mrisho Ngassa, Niyonzima, Nizar Khalfan wakicheza mpira.
Alionekana kuwakera mashabiki na wengine walimzomea. Kipindi cha pili alitumia vyema nafasi alizopata. Aliitendea haki pasi ya Saimon Msuva katika dakika ya 58 na kuifungia Yanga bao la kuongoza na katika dakika ya 66 alifunga bao la pili akimalizia pasi aliyopenyezewa na Kiungo Hassan Dilunga.

Jaja aliupata mpira, akatazama na kufikiria kwa haraka nini cha kufanya. Akakokota mpira kwa hatua moja na kumchambua kiufundi kipa Mwadini Ali,  akinyanyua mpira na kuuzamisha nyavuni.

Uwanja mzima ulilipuka kwa shangwe. Huwezi amini wale wote waliokuwa wanazomea, walishangilia na kuimba jina la Jaja.

Baada ya mechi yule, Jaja aliyekuwa akionekana si lolote, aliimbwa na kusifiwa  sana.

Nilichojifunza ni kidogo tu, mashabiki wa soka huwa wana kiu kubwa ya kuona mchezaji anafanya vizuri na akifanya vibaya wanazomea. Sio Tanzania tu, hata duniani huwa mashabiki wakati fulani wanawachukia washambuliaji wanaposhindwa kufanya vizuri.

Nilisema awali, kazi ya msingi ya mshambuliaji ni kufunga. Kazi ya kwanza ya Jaja ni kufunga. Kumjadili kwa uchezaji wake, sio jambo la msingi.

Kama anacheza kivivu, lakini anafunga, ndio jambo la msingi kwasababu alisajiliwa aje kufunga magoli.

Kama kuna mtu anataka chenga, wapo akina Niyonzima, wataalamu wa vionjo na hata Andrey Coutinho anajua kuuchezea mpira. Kwa Jaja kazi yake ni kufunga.

Mashabiki wa Yanga, Jaja ni mfungaji mzuri kwa mechi nilizomtazama, anajua kukaa maeneo sahihi na kufanya kile afikiriacho.

Wanayanga wakitaka kumuona Jaja akifanya kazi nzuri, wamwache acheze mpira afikiriavyo. Wasimzomee, wamwache awe huru, acheze mdogo mdogo kama afanyavyo, cha msingi ni kufunga.

Kikubwa, Wanayanga, wajifunze kuwaamini wachezaji wao na kukaa pamoja nao pale wanaposhindwa kufanya vizuri. Ni muhimu kujua aina ya staili ya uchezaji kwa wachezaji wote.

Usitake Niyonzima acheze kama Ngassa, hapana, kama mchezaji ana aina ya mpira wake unaoleta matokeo, basi aachwe acheze vile afikiriavyo.


Jaja ataendelea kuwafunga kwasababu ni mchezaji anayejua nini anafanya anapofika langoni. Inawezekana asifunge mabao mengi katika mechi za ligi kuu au akafunga, cha msingi ni kumuamini na kusubiri nini atafanya.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video