Monday, September 29, 2014

Na Baraka Mpenja, Dar es salaam

KADI nyekundu ya Jacob Mwalobo aliwaathiri Prisons kwa kiasi kikubwa, lakini kwa upande wa pili iliwaongezea nguvu zaidi na kuweza kupambana na Yanga iliyokuwa katika morali ya hali ya juu.

Mwalobo alioneshwa kadi mbili za njano na kutolewa nje kwa kadi nyekundu ‘umeme’ kufuatia kurudia kosa kwa kumfanyia madhambi ‘Anko’ Mrisho Khalfan Ngassa.

Wakiwa pungufu walishambuliwa sana, lakini walikuwa imara kuanzia katikati. Walijaa eneo lao na kuwanyima uhuru akina Ngassa, Andrey Coutinho, Jaja, Hassan Dilunga kufika golini kirahisi.

Kipindi cha pili, kocha mkuu wa klabu hiyo, David Mwamwaja, aliwaelekeza wachezaji wake kuwa hawana cha kupoteza, waingie kucheza mpira na kujituma hata kama wako pungufu.

Kweli walikuja juu mno, waligongeana pasi, walipandisha timu juu na kuwapa shida mabeki wa Yanga walioongozwa na Nadir Haroub ‘Cannavaro’ na Kelvin Yondani/Rajab Zahir.

Walipata goli safi la kusawazisha kupitia kwa Ibrahim Kasaka Hassan kutokana na makosa ya mabeki wa Yanga.

Bao hilo liliwaamusha Prisons, lakini wakawa na nidhamu ndogo ya kujilinda na kujikuta wakifungwa goli la pili dakika chache baadaye.

Ilitegemewa kuwa baada ya kusawazisha warudi nyuma kwa muda, watulize akili na kulinda lango lao. Wakishakuwa sawa, waende mbele zaidi kutafuta goli la pili.

Lakini wakisahau kuwa wako pungufu, waliendelea kwenda mbele zaidi baada ya kufunga na kuamini kuwa wanaweza kupata la pili. Ni kweli wangeweza, lakini walitakiwa kuongeza nidhamu ya ulinzi kwasababu walikuwa pungufu.

Kwa kujiamini kwao waliona pointi moja sio ishu, wangeweza kushinda uwanja wa Taifa na kuvuna tatu, ghafla wakafungwa kutokana na kupoteza nidhamu ya ulinzi.

Baada ya mechi, nahodha wa Prisons, Lugano Mwangama alizungumza machache, lakini kubwa aliisifia timu yake kwa kucheza soka safi.

Mwangama alisema: “Tumekubali tumepoteza mchezo dhidi ya Yanga, lakini ni sehemu ya matokeo ya mpira, tunajipanga kwa mechi ijayo, tunakwenda kufanyia marekebisho makosa tuliyoyafanya”.

Akiizungumzia kadi nyekundu ya Jacob Mwalobo katika dakika ya 38 ya kipindi cha kwanza, Mwangama alisisitiza: “Unajua katika mpira tunategemeana na ndio maana ikawekwa idadi ya wachezaji 11 kwa 11, kwahiyo mnapokuwa pungufu, lazima mtapata hitilafu, lakini naipongeza timu yangu, imecheza vizuri, tumeweza kupambana tukiwa pungufu, tumecheza vizuri kiujumla, lakini matokeo hayakuwa mazuri kwetu”.

Baada ya mechi mbili za ugenini, Prisons wanarudi Sokoine Mbeya ambapo Oktoba 4 mwaka huu wataikaribisha Azam fc.

Azam fc watakwenda katika mechi hiyo wakiwa na ushindi wa asilimia 100 katika mechi zao mbili.


Waliifunga 3-1 Polisi Morogoro katika mechi ya ufunguzi na mechi ya pili jumamosi iliyopita waliibamiza 2-0 Ruvu Shootings ya Pwani, mechi zote zilipigwa Azam Complex, Chamazi, Dar es salaam.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video