Thursday, September 25, 2014

Jumanne Athuman Nyamlani (kushoto) akiongea na waandishi wa habari kwenye moja ya mikutano yake siku za nyuma

MICHUANO ya Dr Mwaka SPORTS XTRA NDONDO CUP inatarajia kufunguliwa kesho (septemba 26 mwaka huu) kwa mechi ya ufunguzi baina ya Friend’s Rangers na Kiluvya United.

Mechi hiyo kali itapigwa  uwanja wa Makulumla, Magomeni, Dar es salaam kuanzia majira ya saa 10:15 jioni.

Mgeni rasmi katika mechi hiyo atakuwa Mjumbe wa kamati ya Rufaa ya Shirikisho la soka Afrika, CAF na makamu wa Rais wa zamani wa TFF, Jumanne Athuman Nyamlani.

Michuano hii itakayoendeshwa kwa mfumo wa kisasa kabisa itashirikisha wachezaji wa mchangani kutoka timu 32.

Mbali na dimba la Makulumla, viwanja vingine vitakavyotumika katika mashindano hayo ni Kinesi (Shekilango), Benjamini Mkapa (Ilala) na Mizinga (Kigamboni).

 
Mdhamini Mkuu wa michuano ya  Dr Mwaka Sports Extra Ndondo Cup ,Dr Juma Mwaka akifafanua jambo mbele ya wanahabari kuhusiana na michuano hiyo inayotarajiwa kuanza kutimua vumbi kesho Ijumaa kwenye Uwanja wa Makurumla, Magomeni jijini Dar es Salaam.

Timu 32 zitakazoshiriki zimepangwa katika makundi nane yenye timu nne.


Kundi A: Boom fc, Beira Hotspurs, Tabata fc na Tuamoyo

Kund B: Sifa Politani, Vijana Ilala, Kijichi, Micco Villa

Kundi C: Friend’s Rangers, Temeke Market, Kiluvya United na Muheza fc

Kundi D: Ukonga United, Sinza Stars, Congo Shooting na Snow White

Kundi E: Zakhem, Black Six, TP Same na Makumba

Kundi F: Villa Squad, Scud fc, Nyota Afrika na Burudani fc

Kundi H: Stakishari fc, Abajalo, Shelaton na Kimara United


Kundi G: Temeke United, Sifa United, Forteagle na Segerea fc. 

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video