Monday, September 15, 2014

Kikosi cha Mtibwa Sugar msimu uliopita

MTIBWA Sugar wamesema kitendo cha Yanga kuifunga Azam fc 3-0 katika mechi ya Ngao ya Jamii jana uwanja wa Taifa si kigezo cha kuifunga klabu hiyo katika mechi ya ufunguzi wa ligi kuu soka Tanzania bara, septemba 20 mwaka huu uwanja wa Jamhuri mkoani Morogoro.

Afisa habari wa klabu hiyo, Tobias Kifaru Ligalambwike amesema Azam hawakuwa katika kiwango chao licha ya kuwa na nyota wa ndani na nje ya nchi.

Hata hivyo amewaonya Yanga kuwa ushindi wa jana uliochagizwa na Jaja si sababu ya kuamini kuwa watafanya vizuri uwanja wa Jamhuri Mkoani Morogoro.

“Wasibweteke na ushindi huo na wasiseme tutaanza ligi kwa kasi. Yanga Wampe Maximo miaka mitano ili ajenge timu mpya kwasababu ana kikosi cha watu wazima.” Alisema Kifaru.

“Yanga waliifunga Azam kwasababu walikuwa wagonjwa, hawakuwa katika kiwango chao na ndio maana walifungwa mabao hayo na wangefungwa mengi zaidi.”


“Sikuona kiwango cha Sure Boy,  kijana wangu Himid Mao hakuonekana. Yanga wasijidanganye.”

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video