Sunday, September 14, 2014

Kipre Tchetche kwenye moja ya mechi za Azam fc msimu uliopita

Na Baraka Mpenja, Dar es salaam
SAFU ya ushambuliaji ya Azam fc imemtisha beki na kiungo wa zamani wa Yanga na Taifa Stars, Ally Mayay Tembele kuelekea mechi ya Ngao ya Jamii inayopigwa jioni ya leo majira ya saa 10:00 katika uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam baina ya mabingwa wa ligi kuu msimu uliopita Azam fc na washindi wa pili Yanga sc.

Mayay ameiambia MPENJA BLOG mchana huu kuwa safu hiyo ya ushambuliaji inayoundwa na Mrundi Didier Kavumbagu, Muivory Coast Kipre Herman Tchetche na Mhaiti Leonel Saint Prexu itampa wakati mgumu kocha mkuu wa Yanga, Mbrazil, Marcio Maximo.

“Mimi nakwenda kuona nidhamu ya kiufundi kwa upande wa Yanga, kwasababu Azam ukiangalia kwenye karatasi, safu yao ya ushambuliaji nafikiri ni nzuri kuliko Yanga, lakini ukiangalia kwenye makaratasi.” Alisema Mayay.

“Ukiangalia mtu kama Kipre Herman Tchetche, uwepo wa Mhaiti Leonel Saint Prexu pamoja na Didier Kabumbagu ni hatari sana. Hawa ni washambuliaji watatu wanaoweza kufanya lolote na wakati wowote. Hata kama mwalimua (Omog) atawapanga wote au wawili, bado safu yao ni nzuri ukilinganisha na Yanga”.

“Mtu kama Kavumbagu wakati anahama Yanga ndio kwanza alikuwa ameanza kuwika, kwahiyo nafikiria namna Maximo atavyoweza kuzuia hiyo safu ya ushambuliaji. Njia pekee ya kuzuia ni kukata mipira yote kutokea safu ya kiungo ya Azam fc”.

Mayay ambaye kwa sasa ni kocha na mchambuzi wa soka aliongeza kuwa vipaji binafsi kutoka timu zote pia vinaweza kuamua matokeo.

“Lakini mechi kama hii wakati fulani, uwezo binafsi wa wachezaji unaweza kuamua matokeo. Kila timu inaweza kufuata maelekezo ya walimu kwa asilimia 75 au 80, lakini zinazobaki uwezo binafsi ukatumika.


“Kwa Yanga kuna mchezaji kama Mrisho Khalfan Ngassa, lakini kwa upande wa Azam fc kuna wachezaji vijana, kama beki wa kushoto Gadiel Michael ambaye amekuwa ikiipandisha timu na kutengeneza nafasi”.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video