Monday, September 29, 2014

Mbrazil, Andrey Coutinho (katikati) aliinyoa Prisons goli moja katika ushindi wa Yanga wa 2-1 uwanja wa Taifa 

Na Baraka Mpenja, Dar es salaam

LIGI kuu soka Tanzania bara msimu huu inaonekana kuwa na changamoto tangu mapema.

Mpaka sasa zimechezwa raundi mbili, lakini timu zimenyoana si mchezo. Hebu nikukumbushe namna zilivyonyoa, zilivyonyolewa na kunyoana.

Stand United ikitokea kunyolewa 4-1 na Ndanda fc uwanja wa Kambarage Shinyanga nayo ilimnyoa Mgambo JKT 1-0 uwanja wa CCM Mkwakwani, Tanga.

Prisons ikitokea kuinyoa Ruvu Shooting 2-0 uwanja wa Mabatini, Pwani nayo jana ilinyolewa 2-1 na Yanga.

Yanga akitokea kunyolewa 2-0 na Mtibwa Sugar uwanja wa Jamhuri Morogoro, ilifanikiwa kuinyoa Prisons jana uwanja wa Taifa.

Kagera Sugar ikitoka kunyolewa 1-0 na Mgambo JKT mechi ya ufunguzi Mkwakwani Tanga, nayo iliinyoa JKT Ruvu 2-0 jana, Azam Complex, Chamazi.

Coastal Union ikitokea kunyoana 2-2 na Simba, ilinyolewa 1-0 na Mbeya City iliyoshindwa kunyoana na JKT Ruvu mechi ya ufunguzi.

Polisi Morogoro ikitokea kunyolewa 3-1 na Azam fc uwanja wa Azam Complex Chamazi, ilinyoana 1-1 na Simba jumamosi iliyopita uwanja wa Taifa, Dar es salaam.

Ndanda fc iliyotoka kuinyoa Stand United 4-1 uwanja wa Kambarage Shinyanga, nayo ilinyolewa 3-1 na Mtibwa Sugar uwanja wa Manungu, Complex.

Ruvu Shooting yenyewe imenyolewa mara mbili( 2-0 kutoka Prisons, 2-0 dhidi ya Azam fc).

Timu pekee ambazo zina wembe mkali ni Mtibwa Sugar na Azam fc.

Mtibwa Sugar wamezinyoa timu mbili. Waliinyoa Yanga 2-0 na wikiendi iliyopita wakainyoa Ndanda fc 3-1.

Azam fc nao wamezinyoa timu mbili. Waliinyoa Polisi Morogoro 3-1 na juzi wameinyoa 2-0 Ruvu Shootings.


Ngoja tusubiri kama timu zitaendelea kunyoa, kunyolewa na kunyoana kwa staili hii….

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video