Saturday, September 20, 2014


Jose Mourinho claims clubs who fail to comply with FFP should be thrown out of the Champions League
Jose Mourinho amedai kuwa klabu zinazoshindwa kufuata sheria ya matumizi ya fedha ziondolewa katika michuano ya ligi ya mabingwa 

JOSE Mourinho ameibwatukia Manchester City wakati huu Chelsea akijiandaa kusafiri kwenda Etihad, akidai kuwa UEFA lazima ichukue pointi na kuinyang`anya ubingwa timu inayoshindwa kufuata sheria ya matuzimi ya fedha (FFP).
Bosi huyo wa Chelsea alisema adhabu hiyo itakuwa ya haki zaidi kuliko ya sasa ya kutoza faini na kuizuia klabu kusajili  kama ilivyowakumba City.
"Kila mtu anajua kuwa kuna faini, na kama faini zipo, njia za kuzuia zinakuwepo," alisema Mourinho. "Lakini faini hizo ni za haki? sidhani. Kwa maoni yangu, kitu cha kwanza ni kuondoa pointi na kuondoa ubingwa"
James Milner and Martin Demichelis tackle Arjen Robben during Manchester City's defeat at Bayern Munich
James Milner na Martin Demichelis wakimkaba Arjen Robben wakati wa mechi ya UEFA ambapo Manchester City ilitandikwa bao 1-0 na Bayern Munich

"Kama una mtaji ambao unakufanya umalize tatizo la FFP; halafu unashinda makombe na kutozwa faini, utaendelea kufanya kitu hicho hicho".
Mourinho aliongeza kuwa: "Watamtoa mchezaji mmoja au wawili katika orodha ya UEFA. Halafu badala ya wachezaji 24 unakwenda na wachezaji 22. Lakini kama inaelezwa kuwa utaanza msimu ujao wa UEFA ukiwa umekatwa pointi sita au hutacheza michuanoo ijayo ya UEFA na utakwenda michuano ya Europa, itaonekana kuwa na nguvu'
UEFA waliziadhibu City, Paris Saint-German na Zenit St Petersburg kwa kuvunja sheria ya FFP mwaka huu.
City walitozwa faini ya paundi milioni 50 ingawa inaweza kupunguzwa kama wataifuata baadaye na kikosi chao kinachocheza UEFA mwaka huu kimepunguzwa mpaka wachezaji 21.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video