Wednesday, September 24, 2014

JACOB MASAWE ni miongoni mwa wachezaji wa kutegemewa katika kikosi cha Ndanda fc ya mkoani Mtwara chini ya kocha kijana, Denis Kitambi.
Mwishoni mwa wiki iliyopita, Ndanda fc ikicheza ugenini dhidi ya Stand United katika uwanja wa CCM Kambarage , Shinyanga, Jacob alikuwa miongoni mwa wanandinga walioanza ligi kuu kwa kushindo wakitoa kipigo cha 4-1 kwa wenyeji.

Jacob ambaye ni mdogo wa kocha wa sasa wa Stand United, Emmanuel Masawe, hupendelea zaidi kucheza nafasi ya ushambuliaji wa pembeni, namba 7 na 11, lakini katika mechi hiyo hakuonesha kiwango chake kama alivyozoeleka.

Msimu wa 2010/2011, Jacob alichaguliwa kuwa mchezaji bora wa ligi kuu soka Tanzania bara na mtandao huu umeamua kufanya mahojiano naye. Fuatilia mahojiano haya….

Mwandishi: Mwishoni mwa wiki kwenye mechi ya ufunguzi wa ligi kuu Vodacom Tanzania bara kati ya timu yako ya Ndanda fc dhidi ya Stand United katika uwanja wa Kambarage,  ulikuwa unarejea nyumbani baada ya kuondoka kwa muda,  ulijisikiaje kucheza na timu ambayo ina mazingira ya kinyumbani?

Masawe: Kweli nilijisikia amani sana, kwasababu tangu nimeanza kucheza mpira ligi ligi kuu sijawahi kucheza uwanja wa nyumbani wa CCM Kambarage.

Katika maisha yangu yote sijawahi kucheza mpira nje ya timu ya kaka yangu (Emmanuel) , kwasababu yeye ndiye amenifundisha na kila timu aliyokuwa akifundisha ilikuwa lazima niwepo. Mechi ya jumamosi ilikuwa ya kihistoria katika maisha yangu.

Mwandishi: Ilikuwa ya kihistoria kwa maana gani kwasababu wewe ni mzaliwa wa Shinyanga, umekuwa ukicheza mpira katika maeneo hayo, hususani katikati ya mji, ni kitu gani kilikuzuia kucheza uwanja wa Kambarage kabla?

Masawe: Tangu naingia kucheza ligi kuu, Shinyanga haikuwa na timu yoyote ya ligi kuu na kaka yangu hakuwahi kufundisha timu yoyote ya ligi kuu, kwahiyo nasema ni historia kukanyaga uwanja wa Kambarage. Pia ni mara yangu ya kwanza kukutana na timu tofauti anayofundisha kaka yangu.

Mwandishi: Kabla ya mechi uliwahi kuwasiliana na kaka yako?

Masawe: Sikuwahi kuwasiliana naye kuhusu mpira wakati wa maandalizi zaidi ya kuwasiliana naye kuuliza mambo ya kifamilia, lakini ilikuwa muda kidogo,  siku tano au sita kabla ya mechi hatukuwasiliana kabisa.

Mwandishi: Kabla ya kucheza Ndanda fc, ni timu gani nyingine za ligi kuu umewahi kuzichezea?

Masawe: Timu yangu ya kwanza kucheza ligi kuu ni Toto African, baada ya hapo nikaenda kucheza Africa Lyon na baadaye Mwadui fc. Baada ya hapo nilisajiliwa na JKT Oljoro na sasa niko Ndanda fc.

Mwandishi: 2010/2011 ulikuwa mchezaji bora wa ligi kuu ya Vodacom, ni kipi kilichosababisha ufikie mafanikio hayo na sasa hivi huoni kama ni muda mwingine wa kuchukua tuzo hiyo kwa mara nyingine?

Masawe: Kikubwa kilichonifanya nichukue tuzo mwaka 2010/2011 ni nidhamu niliyokuwa nayo. Cha pili nilikuwa najituma sana hususani nilipokuwa Toto African ambayo ilikuwa timu yangu ya kwanza na nilitamani sana kucheza ligi kuu kabla.

Kwahiyo nikiwa Toto nilicheza kwa nguvu zangu zote na akili zangu zote na ndio maana nikachaguliwa kuwa mchezaji bora. Hapa Ndanda fc naamini nitafanikiwa kwasababu timu ina kila kitu na inabaki kwa mchezaji kujituma.

Mwandishi: Wewe ukiwa uwanjani ni nafasi ipi unafurahia kucheza?

Naifurahia sana nafasi ya mshambuliaji wa pembeni, namba 7 na 11.

Mwandishi: Mchezaji gani anayekuvutia hapa nyumbani na nje ya nchi?

Masawe: Hapa nyumbani anayenivutia sana ni Haruna Moshi ‘Boban’ na nje ya nchi nampenda sana Lionel Messi.



Mwandishi: Unamzungumziaje Denis Kitambi, kocha wa Ndanda fc na ana utofauti gani na makocha waliomtangulia?

Masawe: Kocha kitambi ni mwalimu ambaye yuko karibu sana na wachezaji na anapokuwa kwenye mazoezi unajisikia vizuri.

Ule ukaribu unamfanya kila mchezaji kuwa makini kusikiliza kile anachoelekeza. Tofauti na mazoezini,  anacheka na kila mtu kwasababu ni kijana mwenzetu, inakuwa kama mchezaji vile tofauti na walimu wengine.

Mwandishi: Mechi dhidi ya Stand United hukucheza vizuri kama kawaida yako, ulikuwa na wasiwasi nini?

Masawe: Ni kweli kabisa sikucheza vizuri, lakini kama nilivyokwambia ilikuwa mechi yangu ya kwanza kucheza katika uwanja wa CCM Kambarage nikiwa na timu ya ligi kuu.

 Pia ilikuwa mara ya kwanza kucheza timu tofauti na kaka yangu, halafu nilikuwa nacheza mbele ya familia yangu, rafiki zangu. kwahiyo nilikuwa na kitu kama kauoga hivi, lakini nilitamani nifanye kitu bora na haikuwa hivyo. Huo ndio mpira na nashukuru kwa kile nilichoonesha.

Mwandishi: Kama Mungu angekujaalia kufunga goli ungeshangiliaje?

Masawe: Nisingeshangilia kwasababu mimi ni mmoja wa waanzilishi wa Stand United. Tulipokuwa tunacheza ligi kuu, tukirudi nyumbani tulikuwa na timu yetu ya mtaani iliyoitwa Fanta. Kwa bahati mbaya ikafa na baada ya hapo kulikuwa na mashindano, tukaamua kuunda timu ya Stand kwasababu marafiki zangu wengi wanafanya kazi Stand ya mabasi, kwahiyo tukaona haina budi kuunda timu.

 Nisingeshangilia kwasababu mimi ni mwanzilishi wa Stand, halafu kuna kaka yangu.

Mwandishi: Asante sana Masawe nikutakie maisha mema na Ndanda fc katika msimu huu wa ligi kuu.


Masawe: Nashukuru sana!

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video