Monday, September 29, 2014

Nahodha wa Yanga, Nadir Haroub 'Cannavaro' (wa kwanza kulia, waliosimama wima)

Na Baraka Mpenja, Dar es salaam



KUMKUBALI mpinzani wako pale anapokukaba koo katika soka ni ushujaa mkubwa na inaonesha kuwa wewe ni mshindani wa kweli.

Kuna wachezaji, makocha, viongozi na mashabiki wa soka huwa hawataki kuzungumza ukweli pale timu yao inapofungwa au kushinda.

Siku zote mtu anapenda kusifia chake, hata kama timu yake ilicheza vibaya na kupata magoli, basi atasifia mno. Lakini itakuwa ngumu kusikia akisema tulicheza vibaya ingawa tumeshinda.

Kibongo-Bongo, Simba na Yanga ndio habari ya mjini. Mashabiki wa Yanga wanajasikia furaha sana pale wanapoona timu yao inapata ushindi, hawajali sana namna inavyocheza.

Jana Yanga walichuana na Tanzania Prisons uwanja wa Taifa na kushinda mabao 2-1.

Wakicheza pungufu kwa dakika 52, Prisons walionesha kandanda safi na kuitia presha Yanga hususani kipindi cha pili.

Yanga walijitahidi kucheza vizuri sehemu ya kati na mbele, lakini bado safu ya ulinzi iliyoongozwa na Juma Abdul, David Charles, Nadir Haroub ‘Cannavaro, Kelvin Yondani/Rajab Zahir, iliendelea kuwa na ugonjwa wa kujisahau.

Hata goli walilofungwa jana,  Cannavaro na Yondani walizembea na kumuacha Ibrahim Kasaka Hassan akiruka juu na kupiga kichwa huru kilichomshinda kipa Deogratius Munish ‘Dida’.

Baada ya mechi mashabiki wa Yanga walifurahia ushindi ikizingatiwa walitoka kwenye machungu ya kufungwa 2-0 na Mtibwa Sugar uwanja wa Jamhuri.

Baadhi ya mashabiki walikiri wazi kabisa kwamba wamepata pointi tatu, lakini hali ilikuwa tete kwa upande wa Yanga.

Ghafla wakati wakizungumza hayo, akatokea nahodha wa Yanga na beki kisiki maarufu kama ‘Waziri wa Ulinzi’ wa Yanga, Nadir Haroub ‘Cannavaro’.

Mzanzibar huyu alionesha wazi furaha yake baada ya kuwaongoza wachezaji wenzake kupata ushindi mbele ya timu iliyokuwa bora.

Cannavaro alisema: “Kwanza ni matokeo mazuri. Prisons ni timu nzuri na imeonesha kwamba ina uwezo. Tumecheza na kupata nafasi nyingi, tumepata magoli na tunashukuru kwa kupata ushindi.”

“Siku zote timu ikiwa pungufu inacheza kwa bidii. Wakipungua wanakuja mbele zaidi, na kwasababu na sisi tumeshinda tunalinda goli letu. Walirejesha goli na tukaweza kupata goli la pili, ila Prisons ni timu nzuri na tunashukuru kwamba tumepata ushindi na kusogea mpaka nafasi ya tano”.

“Bado tuna makosa madogo madogo, nadhani kwenye mazoezi tutajirekebisha. Kwenye mechi dhidi ya JKT Ruvu tutaongeza nguvu zaidi”.


Yanga watashuka dimbani tena wikiendi ijayo (Oktoba 5 mwaka huu) kumenyana na JKT Ruvu uwanja wa Taifa, Dar e salaam.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video