Sunday, September 14, 2014

Boniface Pawasa

Na Baraka Mpenja, Dar es salaam

BEKI kisiki wa zamani wa Simba na Timu ya Taifa ya Tanzania, ‘Taifa Stars’, Boniface Pawasa amesema mechi ya Ngao ya Jamii inayopigwa leo jioni uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam baina ya Azam fc na Yanga haitabiriki hata kidogo.

Pawasa amezungumza na MPENJA BLOG muda mfupi uliopita na kueleza kuwa kitakwimu, Azam wapo katika nafasi nzuri zaidi ya Yanga kwasababu timu yao imekaa pamoja kwa muda mrefu, kuliko Yanga chini ya Marcio Maximo.

“Ni mechi ambayo huwezi kuitabiri haraka, lakini ukiangalia takwimu na uzoefu, unaweza kuona Azam wapo katika nafasi nzuri, kwasababu timu yao imeweza kuelewana, juzi juzi ilikuwa katika mashindano ya Kagame. Kwahiyo tayari Azam imeshapata mfumo kwa vile mwalimu wao amekuwa na timu kwa muda mrefu.” Alisema Pawasa.

“Wasiwasi ni mabadiliko ya mfumo wa Yanga, lakini najua Maximo ni mwalimu anayeujua vizuri mpira wa Tanzania, Maximo ni mwalimu mshindani, kwahiyo naamini ana kikosi kizuri, lakini wasiwasi wangu ni timu kombinesheni.”

“Sijaona kama wana kombinesheni bora kuweza kuwapa presha Azam fc, kwamaana nimewaangalia Azam Kagame Cup, ni timu ambayo imeanza kusifika na imeonesha njia. Kwa Yanga mwalimu ana  muda mfupi na timu, lakini siwezi kusema ndio sababu ya kufanya  vibaya”

“Wachezaji ni walewale na kuna wengine wameongezeka, sema mwalimu amekuja na mfumo mpya, kuna mabadiliko, kuna wachezaji walikuwa hawapati nafasi, sahizi wanapata nafasi, leo hii wanacheza mechi ya presha”


“Kwa upande wangu, naangalia uzoefu, takwimu, naona Azam wako vizuri kuliko Yanga”.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video