Sunday, September 21, 2014

Na Baraka Mpenja, Dar es salaam

YANGA SC imeanza vibaya ligi kuu soka Tanzania bara msimu wa 2014/2015 baada ya jana kukubali kipigo cha 2-0 katika mechi ya ufunguzi iliyopigwa uwanja wa Jamhuri mkoani Morogoro dhidi ya wenyeji Mtibwa Sugar.

Ikicheza mbele ya mashabiki waliofurika kutoka Dar es salaam, Morogoro na mikoa ya jirani, Yanga ilionesha kandanda safi na kupata nafasi nyingi za kufunga, lakini washambuliaji wake walichemsha kuzibadili kuwa magoli.

Yanga walicheza mpira mwingi zaidi kipindi cha pili, wakifika golini kwa Mtibwa Sugar, lakini walijikuta wakifungwa magoli mawili kwa staili ya mipira mirefu.

Mussa Hassan Mgosi katika dakika ya 15 kipindi cha kwanza aliwainua mashabiki wa  Mtibwa akifunga bao la kuongoza kufuatia mabeki wa Yanga, Nadir Haroub ‘Cannavaro’ na Kelvin Yondani kushindwa kuosha mpira mrefu uliopigwa langoni mwao.

Yanga waliongoza kumiliki mpira kipindi cha pili, waliikalia barabara Mtibwa na kukaa langoni kwao kwa muda mrefu, huku Mrisho Ngassa na Saimon Msuva wakitumia kasi yao kutokea pembeni na kuwahenyesha mabeki wa timu pinzani.

Wakiwa na matumaini makubwa ya kusawazisha na kuongeza bao la ushindi, Dakika ya 83,  Ame Ali alipata mpira mrefu na kusumbuana na Cannavaro akiwa na mwenzake Yondani, akatishia akapiga mpira wa juu ambapo  kipa Dida alipaa juu na kujaribu kuokoa, lakini ukazama nyavuni na kuiandikia Mtibwa bao la pili.

Goli hilo lilitokana na uzembe wa mabeki wa Yanga ambapo kwa muda mrefu timu yao ilikuwa ikishambulia na mpira ulipopigwa hawakuwa tayari kukuabiliana na shambulizi hilo la kushitukiza.

Baada ya mechi hiyo, watu wengi walitamani kusikia nini atasema kocha mkuu wa Yanga, Mbrazil Marcio Maximo.

Maximo alisema : “Tulicheza mpira na tukafungwa, lakini ligi ndio inaanza. Ninachopenda kusema ni kwamba sio vizuri kupoteza  matumaini kwasababu mechi ijayo tutaweza kuimarika na kushinda”

“Tulipoteza nafasi nyingi, mechi ilikuwa ngumu. Walitumia nafasi zao, sisi hatukutumia nafasi zetu, ni rahisi tu, mpira wa miguu uko hivyo. Ukipoteza nafasi unahatarisha vitu vingi”

“Kitu cha msingi ni kwamba , kamwe timu haitakata  tamaa , huo ndio mpira, wakati fulani siku inakuwa nzuri na siku nyingine inakuwa mbaya”.


Yanga watacheza mechi ya raundi ya pili septemba 28 mwaka huu uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam dhidi ya Tanzania Prisons iliyoshinda jana mabao 2-0 dhidi ya Ruvu Shootings uwanja wa mabatini, Mlandizi, Mkoani Pwani.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video