Friday, August 1, 2014

download
Zinedine Zidane, kushoto, na Claude Makelele, kulia, wanaweza kuzilazimisha timu zao kucheza kama walivyocheza enzi zao.

Na Baraka Mpenja, Kwa msaada wa Mtandao

Imechapishwa Agosti 1, 2014, saa 12:00 jioni

Baada ya mafanikio ya karibuni ya Pep Guardiola, Diego Simeone na Antonio Conte , inaonekana kizazi cha watu waliocheza mpira katika karne ya 20 na 21 kinazalisha makocha bora zaidi.

Zaidi ya makocha watano wanaelekea kuzifundisha klabu kubwa na hapa chini ni matarajio ya msimu wao wa 2014-15.

CLAUDE MAKELELE, BASTIA

Wachezaji wengi bado  wanataka majina yao kuwa kama mchezaji huyu wa zamani, lakini `Makelele’ alikuwa mchezaji mkubwa nchini England kwasababu kiungo huyo wa Ufaransa alionesha kiwango kikubwa na klabu ya Real Madrid na Chelsea.

Nyota huyo alikuwa mahiri kuunganisha kiungo na kama ufundishaji wake unazingatia namna alivyokuwa anacheza, Bastia nzuri na imara inatarajiwa.

Wanahitaji kujiboresha safu ya ulinzi licha ya kumaliza katikati ya msimamo wa ligi msimu uliopita na ilikuwa timu iliyofungwa mabao mengi zaidi. Pengine hii ndio sababu ya Makelele aliyekuwa na sifa ya kulinda kupewa timu.

Mchezaji mkongwe, Mickael Landreau-aliyecheza timu ya Taifa na Makelele-amestaafu na sasa Bastia wamemchukua kwa mkopo Alphonse Areola kutoka PSG, huyu ni kipa wa Ufaransa wa timu ya vijana chini ya miaka 21.

Makelele ana uzoefu mkubwa wa aina ya wachezaji anaotaka kufanya nao kazi. Beki wa kati wa zamani wa Asernal, Sebastien Squillaci amevutia kurudi Ligue 1, kiungo wa Ivory Coast, Romaric na Djibril Cisse wanabaki kuwa wachezaji muhimu.

Pia kuna wachezaji wengine muhimu kama vile Francois Modesto na Mbelgiji aliyesajiliwa kwa mkopo,  Guillaume Gillet wanaweza kuwa msaada mkubwa kwake.

Mchezaji kiongozi uwanjani, mtu anayefanya kazi ya Makelele, Yannick Cahuzac ataimarisha safu ya ulinzi na kwa vile alizaliwa Corsica na kucheza Bastia maisha yake yote ya soka, bila shaka atapata nafasi ya kuwa nahodha.

Makelele atakuwa mvuto mkubwa msimu ujao.


 WILLY SAGNOL, BORDEAUX
Huyu ni mchezaji mwingine wa kimataifa wa zamani wa Ufaransa ambaye amepewa jukumu la kuinoa klabu ya Ligue 1.

Sagnol alikuwa chaguo la pili la Bordeaux, chaguo la kwanza lilikuwa Zinedine Zidane  aliyeichezea klabu hiyo kwa miaka minne katikati ya miaka ya 1990.

Aliamua kuendelea kubakia Real Madrid na Sagnol aliteuliwa badala yake na hii ni baada ya kuonesha uwezo mkubwa akiwa na timu ya Ufaransa ya vijana chini ya umri wa miaka 21 na kuipiga chini kazi ya Lyon.

Kitu kinachovutia kwa kocha huyu ni kwenye mkutano na waandishi wa habari. Alipoulizwa swali kuhusu mchezaji mtukutu, Joey Barton, hakujibu kwa woga.

“Barton, ndiyo, ni mjinga. Hajawahi kushinda chochote, maisha yake ya soka yamejaa matatizo,” Sagnol alijibu mapigo.

Wakati huo huo, havutiwi na maoni ya waandishi wa habari kuhusu timu yake.

“Kwangu mimi, mwandishi hana ufundi inapokuja kwenye suala la mpira, na kocha hajui lolote kuhusu uandishi wa habari,” anasema. “Mara zote naongea na marafiki zangu waandishi. Halafu wanasema, “Tumekuwa tukitazama mechi kwa miaka 20.’ Lakini nimekuwa nikitizama filamu kwa miaka 20, lakini sijawahi kufikia hatua ya kukosoa hata kipande kimoja cha Sinema.”

Baada ya kumaliza nafasi ya 7 msimu uliopita, Sagnol anatarajiwa kumaliza katika nafasi nne za juu.

Magoli yanaweza kutoka kwa mshambuliaji hatari Cheick Diabate, ingawa kuondoka kwa nyota wake, Ludovic Obraniak aliyejiunga na Werder Bremen ni pengo kubwa. Kwasasa Gregory Sertic, kijana mwenye kipaji cha juu ndiye mchezaji mpishi pekee aliyesalia klabuni.

PIPPO INZAGHI, AC MILAN

Miongoni mwa magwiji wa Milan ambao ni pamoja na Alessandro Nesta, Paolo Maldini, Rui Costa na wengineo, hakika usingemfikiria Inzaghi kama ataingia kwenye mambo ya utawala.

Lakini baada ya kuona nusu msimu wa shujaa mwingine wa Milan Clarence Seedorf na kutimuliwa kazi, Inzaghi anarithi mikoba yake kutoka timu ya vijana  ya timu hiyo.

Kurudi kwa Jeremey Menez kumeongoza makali safu ya ushambuliaji ya AC Milan. Menez anaungana na nyota wengine, Stephan El Shaarawy, Mario Balotelli na Keisuke Honda na sasa amejumuika Hachim Mastour ambaye anatarajiwa kupewa nafasi.

Tatizo kubwa la AC Milan ni wachezaji kubadilika badilika na kazi kubwa ya Inzaghi ni kukiunganisha kikosi na kuwapa motisha wachezaji.

 Msimu uliopita Milan walimaliza nafasi ya chini zaidi baada ya kupita miaka 16, sababu si kwamba hawakuwa na wachezaji wenye vipaji. Kazi imebaki kwa Inzaghi kuhakikisha anajenga heshima kuliko Seedorf.

Inzaghi anaonekana kuwa na mfumo wa kumiliki zaidi mpira,pengine sawa sawa na AC Milani ya katikati ya mwaka 2000. Katika mazoezi, amekuwa akisisitiza wachezaji wake kupiga pasi za haraka kwenda mbele ili kushambulia zaidi.

Je, Inzaghi ataendelewa kuwepo AC Milan baada ya msimu ujao? Tusubiri.

COSMIN CONTRA, GETAFE

Kazi kubwa ya Cosmin ni kurudisha nguvu ya Getafe iliyokosa mashabiki wenye mapenzi ya kweli.

Beki huyo za zamani wa kulia wa Getafe, alicheza miaka minne klabuni hapo.

Gentra alikuwa chaguo la kwanza. Alikuwa na msimu mzuri kama kocha huko Romania ambapo alifanya kazi nzuri katika klabu ya Fuenlabrada.

Getafe ni klabu ngeni ambayo uwanja wake umekosa morali na siku zote unakuwa bila mashabiki. Sababu kubwa ni ukosefu wa fedha za kununua wachezaji wakubwa. Ni kazi ya kocha kuwahamasisha wachezaji ili wawe imara kuendana na mazingira halisi.

Hata hivyo, Contra amemsajili Mfaransa Karim Yoda aliyeonesha kiwango kizuri huko Romania, akiisaidia timu yake ya Astra Giurgiu kumaliza nafasi ya pili ambayo hawajahi kushika.

Uimara pekee wa Getafe ni kasi ya washambuliaji wake- kwa mfumo wa Contra, timu hii itakuwa hatari zaidi.

ZINEDINE ZIDANE, REAL MADRID CASTILLA

Zidane pekee katika orodha hii, ndiye kocha anayafanya kazi nje ya ligi kubwa.

Lakini kama sehemu ya kizazi hiki, ni ngumu sana kuridhika na kazi yake ya kuifundisha Real Madrid B. Lakini inaonekana anaandaliwa kumrithi Carlo Ancelotti katika kazi ya kocha wa timu ya kwanza.

Kiukweli, Real Madrid wanamuandaa Zidane kama Barcelona walivyofanya kwa Pep Guardiola.

Kazi kubwa ya Zidane ni kuendeleza vipaji changa na pengine atamkuza zaidi mtoto wake mwenye miaka 19, Enzo ambaye anatumia jina la ukoo wa mama yake, Fernandez.

Enzo amepandishwa kutoka Juvenil A mpaka kikosi cha Castilla kwa ajili ya msimu wa 2014-15, akivaa jezi namba 10 aliyokuwa anavaa Zidane akiwa na timu ya Real Madrid na Ufaransa na amekuwa akicheza kama baba yake, hususani kumiliki mpira na kupiga krosi.

Pia watoto watatu wa Zidane,--Luca miaka 16, Theo (12) na Elyaz (8) wapo katika akademi ya Real Madrid, hivyo atafanya nao kazi.


Lakini nani anajua? Muongo mmoja ujao, Zidane anaweza kuwa kocha wa timu ya wakubwa ya Real Madrid akiwa na watoto wake wanne kwenye kikosi.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video