Saturday, July 19, 2014

Kocha wa Tanzania Prisons, David Mwamwaja akiwa kazini

Na Baraka Mpenja, Dar es salaam


Imechapishwa Julai 19, 2014, saa 2:40 usiku

MAAFANDE wa jeshi la Magereza, Tanzania Prisons, maarufu kwa jina la `Wajelajela` wameamua kupunguza kasi ya mazoezi baada ya shirikisho la soka Tanzania, TFF, kusogeza mbele ligi kuu soka Tanzania bara mpaka septemba 20 mwaka huu.

Kocha mkuu wa klabu hiyo, Mkongwe, David Mwamwaja amesema walianza mazoezi mwezi wa sita na walikuwa wanachambua wachezaji ili wajiunge na timu yao.

“Zoezi la kuchambua wachezaji lilienda vizuri na likaisha, lakini sasa limekuja suala la kuahirisha ligi, tumeona tupunguze mazoezi kwasababu hamu ya mpira kwa wachezaji itapungua”

“Nafikiri tutapata nafasi ya kumpuzika ili kupata nguvu mpya,” . Alisema Mwamwaja.

Kocha huyo alisema amefanya usajili wa wachezaji wawili tu kwasababu anao vijana wengi aliowapandisha kutoka kikosi cha vijana chini ya miaka 20.

“Nimemsajili mshambuliaji Amir na mlinda mlango, Mohamed kutoka JKT Oljoro. Hawa wananitosha na nimezingatia uhitaji wangu”. Alisema Mwamwaja.

Kwanini ameamua kusajili wachezaji wawili na kuwapandisha vijana, Mwamwaja alisema kwamba ligi kuu inatisha kwa jina tu, lakini ni mpira wa kawaida, wachezaji ni wale wale, hivyo ameamua kuchukua wachezaji kwa nafasi anazohitaji.

Kocha huyo alisema msimu ujao anatarajia kupata nafasi za juu zikiwemo nafasi ya ubingwa, nafasi ya pili au tatu.

Msimu uliopita, Prisons walinusurika kushuka daraja na walifanikiwa katika mchezo wa mwisho dhidi ya Ashanti United.

Walimaliza katika nafasi ya 10 kwa kujikusanyia pointi 28 kibindoni, hivyo kuwaachia majanga ya kushuka daraja, wauza mitumba wa Ilala, Ashanti United, Maafande wa JKT Oljoro na Rhino Rangers.


Nafasi za timu hizo tatu zilizoshuka daraja zimechukuliwa na Polisi Morogorogo ya Morogoro, Stand United ya Shinyanga na Ndanda fc ya mkoani Mtwara.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video