Sunday, July 20, 2014

Mbwana Samatta (kushoto) na Mrisho Ngassa (kulia) wataanza pamoja

Na Baraka Mpenja, Dar es salaam


Imechapishwa Julai 20, 2014, saa 7:00 mchana

TAIFA STARS chini ya kocha Mholanzi, Mart Nooij inaingia uwanjani jioni ya leo kuvaana na Msumbaji (Black Mambas) katika mchezo wa kuwania kupangwa hatua ya makundi ya kusaka tiketi ya kushiriki fainali za mataifa ya Afrika, AFCON, mwakani nchini Morocco.

Stars yenye bunduki zake zote itakabiliana na Mambas wenye historia ya kuiharibia katika michezo muhimu kwani waliwahi kufungwa bao 1-0 uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam mwaka 2007 kuwania kucheza fainali za AFCON , mwaka 2008 nchini Ghana.

Pia mwaka 2012, Msumbiji waliitoa Stars chini ya Kim Poulsen kwa mikwaju ya penati kuwania kucheza AFCON mwaka 2013 nchini Afrika kusini..

Kuelekea katika mchezo huo, kocha mkuu Mart Nooij alisema maandalizi yamekamilika na wanasubiri muda ufike ili wakaoneshe walichojiandaa katika kambi ya Botswana na mjini Tukuyu mkoani Mbeya.

Wachezaji wote wamesema wapo tayari kwa mechi ya jioni ya leo ambapo Mbwana Samatta alisema yuko fiti kwa asilimia 100 na ataisaidia Stars kuibuka na ushindi.

10357474_634079413340945_8148690486284095511_n
Naye Thomas Emmanuel Ulimwengu alisema mechi itakuwa ngumu, lakini wapo katika morali ya kufanya kazi kwa umoja zaidi uwanjani, huku akiwaomba watanzania kujitokeza kwa wingi kuishangilia timu yao.

Beki Shomary Kapombe yeye alisema kambi ya Tukuyu imekuwa na matunda  kwasababu wachezaji wote wapo katika morali ya kutafuta ushindi. Hata hivyo aliwaomba mashabiki kufika kwa wingi kuwaongezea hamasa ya ushindi.

Kocha Mart Nooij anahitaji ushindi si chini ya mabao 3-0 ili kujiweka mazingira mazuri ya kusonga mbele katika mchezo wa marudiano wiki mbili zajazo mjini Maputo nchini Msumbiji.

Katika mchezo wa leo, Nooij amewaanzisha washambuliaji wanne, Mbwana Ally Samatta, Thomas Emmanuel Ulimwengu, John Raphael Bocco `Adebayor`  na Mrisho Khalfani Ngassa `Anko`.

Mlinda mlango ataendelea kuwa Deogratius Munish `Dida`, huku mbavu ya kulia ikikamatwa na Shomary Kapombe.

Upande wa kushoto atasimama Oscar Samwel Joshua, wakati vitasa vya kati ni Kevin Yondan na nahodha Nadir Haroub `      Cannavaro”.

Safu ya kiungo atasimama Erasto Edward Nyoni na Mwinyi Kazimoto Mwitula.

Nyoni amechukua nafasi ya kiungo majeruhi, Frank Domayo `Chumvi`. Kikosi cha Nooij hakijawa na mabadiliko ukilinganisha na kile kilichoifunga Zimbabwe bao 1-0 ndani ya dimba la Taifa.

Thomas Ulimwengu (kushoto) anawaonesha kazi Mambas jioni ya leo

Katika mchezo wa leo, kocha wa Stars anatarajia kucheza mpira kwa mfumo wa kulinda lango, kumiliki mpira na kushambulia kwa kasi.

Ni muhimu kuwazuia Msumbiji kupata bao lolote la ugenini, hivyo mabeki wanatakiwa kukaba nafasi na kuwafanya Msumbiji wasicheze mpira wanaotaka.

Mabeki wana  kazi ya kuwafanya washambuliaji wa Msumbiji washindwe kutekeleza mipango yao. Stars inahitaji kumiliki mpira kwa muda mrefu na kutengeneza mashambulizi.

Kazimoto ana kazi ya kuwachezesha washambuliaji wa Stars. Mashambulizi ya kasi na makini yataifanya Stars ipate matokeo jioni ya leo.

Nao mashabiki wana wajibu wa kuishangilia timu kwa muda wote ili vijana wawe katika hamasa kubwa.


Kila la kheri Taifa stars kuelekea mchezo muhimu jioni ya leo.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video