Sunday, July 20, 2014

mm
Na Baraka Mbolembole
Azam FC ilianzishwa mwaka 2007, lakini timu hiyo ilikuwepo tangu mwaka 2004 ikiwa chini ya wafanyakazi wa kiwanda . Awali timu hiyo ilikuwa ikifahamika kama Mzizima FC, ingawa ilianzishwa kwa lengo  la kuwafanya wafanyakizi kujiweka vizuri kiafya, timu hiyo ilikuwa ikishiriki katika ligi daraja la Tatu, Manispaa ya Ilala hadi mfumo huo wa madaraja ulipoondolewa mwishoni mwa mwaka 2005.

Wazo la Abubakary Bakhressa kuanzisha timu kabambgi daraja la Tatu, Manispaa ya Ilala hadi mfumo huo wa madaraja ulipoondolewa mwishoni mwa mwaka 2005.

Wazo la Abubakary Bakhressa kuanzisha timu kabambeyo ilikuwa ikihusisha mabingwa wa Mikoa. Mara baada ya kupanda ligi kuu, Azam FC ilifanya usajili wa wachezaji nyo walioshika nafasi ya pili, na Simba  ubingwa.

Msimu wake wan ne katika ligi kuu timu hyo  ilifanikiwa kumaliza katika nafasi ya pili nyuma ya waliokuwa mabingwa Simba SC kwa tofafauti ya pointi mbili. Baada ya kuipiga kumbo Mtibwa Sugar katika misimu miwili ya nyuma katika nafasi ya tatu, safari hii Azam iliwaondoa Yanga na kuwa miongoni mwa timu mbili za juu.

Baada ya kupiga hatua hiyo na kupata nafasi ya kuiwakilisha nchini katika michuano ya Kimataifa, Azam iliendelea kupandisha ubora wake wa kiuchezaji na kimipango na kufanikiwa kwa mara nyingine kumaliza katika nafasi ya pili katika msimu wa 2012/13 nyuma ya Yanga ambao walitwaa ubingwa huo. Simba ilitupwa nje ya timu mbili za juu.

11
MSIMU WA MAFANIKIO

AZAM FC ilitwaa ubingwa wake wa kwanza wa ligi kuu Tanzania Bara katika msimu wa 2013/14 ukiwa ni msimu wao wa sita tangu walipopanda ligi kuu. Ni mafanikio makubwa lakini kote huko kuna njia ngumu ambayo wamepitia. “ Msimu wa 2014/14 ndiyo msimu wetu bora kwa kuwa tulifanikiwa katika malengo yetu” anasema meneja wa timu hiyo. Jemedari Daid

 “  Tulikuwa na melengo mawli, Kwanza ilikuwa ni kuhakikisha  tunafanya vizuri na walau kufika robo fainali katika michuano ya kombe la shirikisho baani Afrika, na lengo la Pili ilikuwa ni kutwaa ubingwa wa ligi kuu. Tulifanikiwa katika lengo la Pili na tulitolewa mapema katika michuano ya Shirikisho na timu ya Ferreviaro Beira ya Msumbiji. Tulishinda mchezo wa kwanza nyumbani kwa bao 1-0 na tukafungwa mabao 2-0 ugenini. Mara baada ya kutolewa katika michuano hiyo tulielekeza nguvu zetu katika ligi kuu na tulifanikiwa kutwaa ubingwa”

Swali; Azam iliwezaje kutwaa ubingwa”

JEMEDARI; Kuwa bingwa hakukuja tu, tulikuwa na ‘ plan’ ya muda mrefu kidogo. Baada ya kumaliza katika nafasi ya Tatu kwa misimu miwili ( 2009/10-2010/11) na kumaliza katika nafasi ya Pili mara mbili (  2011/12-2012/13, tuliweka malengo ya kuhakikisha tunatwaa ubingwa msimu uliofuata. Nachoweza kusema ni kwamba Mwalimu, Stewart Hall amechangia kwa asilimia kubwa ubingwa wetu msimu uliopita. Nampa asilimia 65 hadi 70 kuwa alifanikisha ubingwa . Ukizungumza wa weledi, timu inapitia sehemu mbili muhimu ili kuelekea katika ubingwa.

IMG_3174
Kwanza, ni kwenye usajili, Pili ni kwenye maandaalizi. Ukifeli katika usajili na maandalizi huwezi kuwa bingwa, Mwalimu, Hall ndiye aliyeshiriki kwa asilimia kubwa katika kusajili timu na ni yeye aliyefanya maandalizi mazuri. Kabla ya msimu kuanza Mwalimu, Stewart alikaa na wachezaji wote pamoja na viongozi wa klabu na akawaeleza nia yeke ya kutwaa ubingwa.

Tarehe 9, julai, 2013 kulifanyika kikao kati ya benchi la ufundi na wachezaji wote , ilikuwa ni kabla ya mchezo wa kirafiki dhidi ya timu ya Kombaini ya Polisi Tanzania katika mchezo wa kirafiki ndani ya uwanja wa Taifa. Nakumbuka mchezo huo tulishinda kwa bao 1-0 lililofungwa na Ladson Kakolaki Hall aliwaambia kwa nini wanataka kuwa mabingwa. Ni sehemu zipi ambazo tuzifanyie kazi ili kuwa mabingwa.

SWALI; Mlichukuliaje changamoto ya misimu iliyopita?

JEMEDARI;  Msimu ambao Simba SC walikuwa mabingwa tulizidiwa kwa pointi sita, na msimu uliofuata ambao Yanga walikuwa mabingwa tulikuwa nyuma kwa pointi sita pia, lakini  tulikuwa na pointi 56 katika michezo yote ya msimu, Hall akatuambia kuwa ili kuwa bingwa wa ligi kuu ni lazima uwe na pointi 60 hadi 61 kwa hiyo alisema tuongeze point inane katikac zile 56 na tutakuwa mabingwa. Tunawezaje kupata pointi hizo?

Stewart aliwaelekeza viongozi na kuwaambia kuwa kuna maeneo ni lazima yaboreshwe. Kwanza ni ‘ U-proffesionalsm’ ni lazima tuongeze kwa asilimia tano, ‘ fitness’  tuongeze pia kwa asilimia tano na akawaambia wachezaji kuwa eneo lingine ni katika ‘ ufundi na mbinu’  alihitaji pia tuongeze kwa asilimia tano.

IMG_3132
Katika ‘ Fitness’  alishauri tumuajiri mtu ambaye ana uwezo na mtaalamu wa idara hiyo na akaajiliwa Mtu sahihi kutoka nje ya nje. Wachezaji wamekuwa na vipindi maalumu katika siku za Jumatatu, Jumatano na Ijumaa kulikuwa na ‘ section’ moja moja ya gym ili kuongeza nguvu kwa wachezaji. Aliwashauri wachezaji wazawa kucheza mpira kama wachezaji wa kulipwa na kuachana na mambo ambayo yatawafanya kuwa nje ya kazi yao. Aliwambia anafahamu wanaishi nyumbani  lakini wanapaswa kupunguza sababu ambazo zinawafanya wawe nje ya timu kama sababu za ‘ mtoto au mzazi kuumwa ‘ . Aliwaambia watambue kuwa wapo kazini na kuna watu wanawategemea. Alitaka wachezaji wote wasikose mazoezini.

Aliwataka wachezaji waboreshe ufundi wao binafsi, pia aliwataka kufuatilia mafundisho na melekezo yote ya kiufundi ambayo watakuwa wakipewa. Hivyo ukiunganisha asilimia hizo 15 na kuongeza pale tulipokuwa tumeishia katika misimu miwili ya mwisho tungeweza kabisa kupata pointi hizo nane hadi kumi na kutwaa ubingwa.

SWALI;  Je, ujumbe huo ulifika ipasavyo kwa wachezaji?

JEMEDARI; Tunashukuru wachezaji walimuelewa japo kuwa mwanzoni wakati wa maandalizi kuna wanachezaji walionekana kusuasua, tulianza maandalizi Juni 24, 2013 ambayo yaliwahusisha wale wachezaji wasiokuwa na majukumu yoyote katika timu za Taifa. Wale wachezaji ambao walikuwa katika timu za Taifa walipewa wiki mbili za mapumziko

Wachezaji wa kigeni wao walipewa ruhusa wiki moja kabla ya wachezaji kuondoka. Nakumbuka mchezo wa mwisho wa ligi ambao tulicheza Arusha ( dhidi ya JKT Oljoro msimu wa 2012/2013) wachezaji wote wan je walikuwa tayari wamepewa ruhusa ya kurudi nyumbani kwao. Hivyo walitakiwa kuwahi maandalizi ya msimu mpya baada ya wiki moja, hivyo katika wiki ya pili wote walikuwa tayari wamewasili.

IMG_3202
Baada ya hapo tulicheza michezo mingi ya kujipima nguvu katika uwanja wetu wa Azam Complex Chamanzi. Tulianza kucheza michezo ya kirafiki na timu za kawaida, tulicheza na African Lyon mara mbili, timu yetu ya Pili, kabla ya tarehe 4, agosti kusafiri kwenda Afrika Kusini kucheza michezo minne ya kujiandaa na msimu. Nachoweza kusema ‘ pre-season’ yetu yote ilikuwa kule.

Wakati tupo kule Mwalimu alipendekeza mtu mmoja anayeitwa Taylers ambaye alisafiri kutoka London, England na kuunga nasi tukiwa kule.  Mechi yetu ya kwanza tulicheza na Kaizer Chiefs jijini , J,burg na tulipoteza kwa magoli 3-0.

SWALI; Kuna kitu ambacho mlijifunza baada ya mchezo huo?

JEMEDARI; Mechi ile ilitufunza mambo mengi, ilionesha tofauti kubwa kati yetu na wao. Baada ya mchezo ule tulikwenda katika uwanja wa mazoezi na wachezaji wote na kila mchezaji alikiri kuwa wenzetu wapo mbali zaidi ya tulipo sisi, unajua wachezaji nao ni binadamu hivyo baada ya kuona wamepata kuwa washindi wa pili mara mbili katika ligi ya nyumbani wengine wanaweza kujiona ni wachezaji wakubwa. Lakini baada ya kipigo kile kutoka kwa Kaizer kila mmoja aliona udhaifu wake, ilikuwa mechi ambayo Kaizer walitumia vijana wa timu yao ya Pili kwa asilimia kubwa kuliko wale wa kikosi cha kwanza.

Walitumia wachezaji wane ambao hawakuwa wakipata nafasi sana katika michezo ya ligi kuu ya Afrika Kusini, lakini kile ambacho walikifanya na tulichokishuhudia kila mtu kila mpa nafasi ya kujiuliza mara mbili mbili. Tulijiuliza ni kweli ni ‘ sisi washindi wa pili mara mbili mfululizo katika ligi kuu ya Tanzania Bara’ au? Ni, kweli tulikuwa tayari kufika robo fainali ya michuano ya CAF?. Kila mmoja alishtuka na kujiuliza maswali mengi.

ccc
Kitu kizuri tulikwenda pale kujifunza na kila mchezaji alikubali kuwa kiwango chetu kipo chini. Tulijua kuwa mechi zote zitakazofuata zitakuwa kama ile ( dhidi ya Kaizer) lakini bahati nzuri baada ya siku mbili tukacheza na Mamelod Sundown ( mabingwa wa mwaka jana wa PLS) Tukacheza nao katika uwanja wao wa mazoezi tukafanikiwa kuwafunga kwa bao 1-0 ambalo lilifungwa na mshambulizi, Gaudensi Mwaikimba.

Kocha wa Sundown, Pitso Mosimane, na meneja wa timu hiyo Peter Ndlovu ( mchezaji wa zamani wa kimataifa wa Zimbabwe)  Walifanya mahojiano na sisi na kutuuuliza tupo katika nafasi gani katika ligi kuu, tukawaambia kuwa sisi ni washindi wa pili mara mbili mfululizo. Wakatuambia kuwa kama tutaendelea kucheza kama ilivyokuwa katika mchezo ule dhidi yao basi tungekuwa na nafasi kubwa ya kuwa mabingwa katika ligi . Kitu ambacho kilikuja kutokea kweli baadae.

Mechi ya tatu tulicheza na Orlando Pirates ambao walikuwa wakicheza klabu bingwa Afrika hivyo walileta wachezaji mchanganyiko kutoka timu ya kwanza na ile ya pili. Tulipoteza mchezo hule kwa mabao 2-1, mechi ile ilikuwa ngumu sana lakini tayari tulikuwa tumeanza kuzoea kucheza dhidi ya timu za Afrika Kusini. Mechi ile nakumbuka ilitugharimu sana kwani tulicheza katika hali ya baridi kali na mvua kubwa ambayo ilinyesha usiku wa kuamkia siku ya mchezo ambao tulicheza asubuhi.

Baada ya mchezo huo tulikwenda Soweto kucheza na Maroka Swallows tukafungwa goli 1-0 lakini ni mechi ambayo tuliona uwezo wa golikipa wetu mdogo, Aishi Manula, licha ya Swallows kufunga goli moja kijana huyo alifanya kazi kubwa sana. Mechi mbili alicheza Mwadini Ally kipa wetu mzoefu na mbili alicheza Aishi na kutokana na kiwango alichokionesha Aishi, Mwalimu, Stewart aliona hakuna sababu ya kumpanga Mwadini katika mchezo wetu wa ufunguzi wa msimu ‘ Ngao ya Jamii’ dhidi ya Yanga ambao ulichezwa tarehe 17, agosti, 2013.

1_1
Mwalimu alisema kuwa Mwadini alikuwa amepita kipindi kigumu sana, kwani tangu alipocheza mchezo wa mwisho wa ligi kuu msimu wa 2012/13 hakuwa amecheza mchezo wowote katika timu ya Taifa, hivyo kutokana na Mwadini kuonekana kukosa ‘ match fitness’ Mwalimu alifanya maamuzi ya kumtumia, Aishi katika mchezo dhidi ya Yanga.

SWALI; Baada ya kurudi nchini nini kiliendelea?

JEMEDARI; Tulicheza mchezo wa kwanza dhidi ya Yanga katika Ngao ya Jamii na kufungwa kwa goli 1-0. Tulianza ligi kwa kucheza na Mtibwa Sugar na kulazishwa sare ya kufungana bao 1-1 katika uwanja wa Manungu, tukaenda Tabora kucheza na Rhino na kushinda kwa mabao 2-0 na tukaenda Bukoba kucheza na Kagera Sugar, na kutoka sare ya kufunga bao 1-1. Na kabla ya kupisha kambi ya timu ya Taifa tulicheza na Ashanti United na kupata sare ya bao 1-1.

Hayakuwa matokeo mazuri sana kutokana na maandalizi ambayo tuliyafanya. Tuliamini namna timu nyingine zilivyokuwa zimejiandaa na maandalizi tuliyokuwa tumeyafanya kwa upande wetu tulistahili kupata matokeo bora zaidi ya hayo. Tulifikiri mechi ya Ashanti ilikuwa ni lazima tupate matokeo baada ya kushindwa kufanya hivyo dhidi ya Mtibwa na Kagera katika viwanja vya ugenini. Mchezo dhidi ya Ashanti ambao ulikuwa wa kwanza katika uwanja uwanja wa nyumbani, Azam Complex Chamanzi, ulituongezea machungu zaidi.

azam goalz (1)
Hali haikuwa nzuri sana na tukaanza kupata wasiwasi, siyo kutokana na matokeo tu ya uwanjani bali namna timu ilivyokuwa ikicheza tulipatwa na wasiwasi kwa kuwa mchezo uliokuwa ukifuata ulikuwa dhidi ya Yanga ambao tayari walikuwa wametufunga katika mchezo wa Ngao ya Jamii, lakini tukaona baada ya pale kuna unaliza wa kuwatumia wachezaji wa timu ya Pili.

Kwa mara ya kwanza katika kikosi cha wachezaji 18 kulikuwa na wachezaji watatu wa Academy yetu. Farid Mussa Shaa. Joseph Kimwaga ambaye alifunga goli la ushindi katika dakika ya mwisho ya mchezo, na  Leonard Luis Mlingila. Katika mchezo ule Farid alianza kama winga wa kushoto na wengine walikuwa katika benchi. fArid alifanya vizuri na ndiye alitoa krosi ya goli la kwanza, alipotoka  na kumpisha Kimwaga ambaye alikuta matokeo yakiwa sare ya mabao 2-2 alifunga bao zuri la ushindi. Tukaanza kuwaamini vijana wa timu yetu ya Pili na kuona tuna hadhina kubwa. Tulitumia vijana zaidi ya saba kwa msimu mzima.

Gabriel Michael ambaye alikuwa mchezaji wa kutegemewa katika raundi ya pili kama mlinzi wa kushoto, Kelvin Friday na Yahaya Abbas ni vijana wengine ambao walipandishwa katika timu ya kwanza kutoka katika Academy na walitoa mchango mkubwa kwa timu.

MATOKEO YA AZAM  FC MZUNGUKO WA KWANZA

Azam ilitwaa ubingwa baada ya kufikisha pointi 62 katika mi8chezo 26, walianza msimu kwa sare mfulizo dhidi ya Mtibwa Sugar katika uwanja wa Manungu, Turiani. Katika mchezo huo wa kwanza, Azam ikiwa chini ya kocha Stewart Hall ililazimisha sare ya kufungana goli 1-1 goli la vAzam katika mchezo huo lilifungwa na mlinzi, Aggrey Morris, hihi ilikuwa ni  septemba 24 na siku nne baadae, waliichapa Rhino Rangers kwa magoli 2-0 katika uwanja wa Ali Hassan Mwinyi, Tabora. Magoli ya Kipre Tcheche yaliwapatia ushindi wao wa kwanza wa msimu tena wakiwa ugenini.

azam bingwa
Walianza mwezi oktoba kwa sare ugenini dhidi ya timu ngumu ya Kagera Sugar katika uwanja wa Kaitaba, Bukoba. Sare ya kufungana goli 1-1 ilionekana ni kama timu hiyo haina uwezo wa kutwaa ubingwa lakini ilikuja kuonesha umuhimu wake wakati ligi ikiwa ukingoni huku timu zikipishana pointi chache. Pointi moja ya Kagera ilikuwa muhimu. Hamis Mcha ‘ Vialli’ ndiye alikuwa mkombozi katika mchezo huu baada ya kufuta goli la Themi Felix na kuisawazishia timu yake


Katika mchezo wa kwanza ndani ya uwanja wake wa nyumbani, Azam ilijikuta ikilazimishwa sare na Ashanti United ambao walikuwa wamepoteza michezo yote mitatu ya mwanzo. Mlinzi wa United na mchezaji wa zamani wa Azam, Tumba Sued aliswazisha goli la  Kipre Tcheche dakika tano kabla ya kumalizika kwa mchezo na kufanya timu hizo kufungana goli 1-1 . Hali hiyo ilianza kutia shaka kama ni kweli timu hiyo ingeweza kumaliza katika nafasi mbili za juu achilia mbali kutwaa ubingwa. Hakika mwezi, oktoba ulikuwa mgumu sana kwa timu hiyo kwa kuwa haikupata ushindi wowote katika michezo minne mfululizo.

Baada ya sare dhidi ya Kagera Sugar na Ashanti United, Azam ilisafiri hadi jijini, Mbeya kuikabili Tanzania Prisons na kwanyingine Tcheche akawa mwokozi wa timu hiyo pale alipofunga goli pekee la Azam katika sare ya kufungana goli 1-1. Azam walibanwa na ratiba katika raundi ya kwanza nap engine jambo hilo liliwafanya kupata matokeo ambayo yalionekana mabaya. Walikwenda jijini, Tanga na kulazisha suluhu-tasa dhidi ya Coastal Union.

Baada ya kuambulia pointi nne katika michezo minne ya mwezi, oktoba, Azam ilirejea katika uwanja wake wa Azam Complex Chamanzi, na kuichapa timu ya JKT Mgambo ya Tanga kwa magoli 2-0. Washambuliaji waliokuwa majeruhi, John Bocco na Mganda, Brian Omony walifunga magoli yao ya kwanza katika msimu wa 2013/14 na kuisaidia timu yao kuibuka na ushindi wa pili wa msimu katika michezo saba.

SAM_2252
Kiungo, Mkenya, Humphrey Mieno, mlinzi, Erasto Nyoni na kiungo Salum Abubakary ‘ Sure Boy’ kila mmoja alifunga goli lake la kwanza la msimu wakati Azam ilipoichapa JKT Ruvu kwa magoli 3-0 katika uwanja wa Azam Complex Chamanzi. Mwezi novemba ulikuwa mzuri kwa kikosi cha Hall, na walikwenda Arusha na kuibuka na ushindi wa goli 1-0 dhidi ya JKT Oljoro, mshambulizi Bocco ndiye alikuwa mfuingaji wa goli pekee katika mchezo huo.

Kwa mara nyingine, Bocco na Mcha wakaibuka katika orodha ya wafungaji wakati walipoisadia timu yao kuichapa Simba SC kwa magoli 2-1. Kitendo cha kuifunga Simba ilikuwa ni dalili za timu hiyo kuonesha ipo tayari kupambana kuwania taji japokuwa hakufanya vizuri katika michezo mitano siku za nyuma.

Wakaichapa Yanga SC isivyotarajiwa kwa magoli 3-2, Kipre, Mcha, na chipukizi Joseph Kimwaga walikuwa wafungaji wamagoli ya Azam katika mchezo huo uliokuwa mkali na wa kusisimua.  Bocco, Erasto, na Sure Boy walikuwa wafungaji wa magoli ya Azam wakati ilipoichapa Ruvu Shooting kwa magoli 3-0 katika uwanja wa Azam Complex Chamanzi. Azam FC ilimaliza mzunguko wa kwanza kwa kulazimishwa sare ya ‘ajabu’ katika uwanja wa nyumbani dhidi ya Mbeya City. Azam ililazishwa sare ya kufungana magoli 3-3, Mcha, Tcheche na Mieno walikuwa wafungaji wa Azam wakati, Mwigane Yeya alifunga magoli yote ya City siku hiyo . Katika michezo 13 walikusanya pointi 26.

MATOKEO MZUNGUKO WA PILI

Azam FC, ilianza duru la pili la ligi kuu Tanzania Bara kwa ushindi mwembamba wa goli 1-0 dhidi ya timu ya Mtibwa Sugar. Bao pekee katika mchezo huo lilifungwa na mshambulizi, Kipre Tcheche. Wakashinda michezo mingine mitatu kati ya minne waliyocheza katika mwezi wa pili,
baada ya kuifunga Mtibwa, walizichapa timu za JKT Oljoro, Kagera Sugar katika uwanja wa Chamanzi. Kipre baada ya kufunga katika michezo miwili dhidi ya Mtibwa na Rangers, safari hii ni Brian Omony kiungo-mshambulizi wa kimataifa wa Uganda aliyefunga mara mbili, kinda Kelvin Friday akafunga bao lake la kwanza katika ligi kuu, na kiungo Jabir Aziz akahitimisha ushindi wa mabao 4-0 dhidi ya Kagera.


Azam ilishuhudia Tanzania Prisons ikipata sare ya kufungana mabao 2-2.  Aggrey Morris katkulazimishwa sare, AzamFC iliibuka na ushindi mwingine   ' mnono' wa mabao 4-0 mbele ya Ashanti United.. Aggrey, na patna wake katika safu ya ulinzi, Said Mourad walifunga bao moja kila mmoja na mshambulizi, Gaudensi Mwaikimba akafunga mara mbili katika mchezo huo.


Kipre  alifunga bao moja, Friday alifunga bao lingine moja, nahodha John Bocco akafunga mara mbili katika mchezo huo dhidi ya Coastal Union. Baada ya mchezo huo Azam ilikutana na waliokuwa mabingwa watetezi wa taji, Yanga katika uwanja wa Taifa. Na kulazimisha sare ya bao 1-1, kinda Friday alisawazisha dakika tano kabla ya mchezo kumalizika na kulinda uongozi wa tofauti ya pointi nne baina yao na Yanga.


Wakaifunga Simba kwa mabao 2-1. Mabao yote yakifungwa na Kipre Tcheche. Walikwenda Arusha kucheza na JKT Oljoro na kiungo wa pembeni Hamis Mcha alifunga bao pekee katika ushindi wa bao 1-0. Baada ya mchezo huo wa Arusha, ligi kuu ilikuwa imesalia na michezo mitatu na Azam waloikwenda Mlandizi, Pwani kucheza na Ruvu Shooting na kuibuka na ushindi wa mabao 3-0. Mwaikimba, Himid Mao ambaye alifunga kwa mara ya kwanza, na Kipre walikuwa wafungaji wa mchezo huo. WAkaifunga JKT Mgambo kwa mabao 2-0 kinda Farid Mussa alifunga bao lake la kwanza na kuungana na Kimwaga, na Friday kisha Kipre alifunga bao lake la 12 la msimu.


Azam FC waliichapa Mbeya City katika uwanja wa Sokoine, Mbeya kwa mabao 2-1 na kujihakikishia taji la kwanza la ligi kuu baada ya miaka sita. Bocco alifunga bao la ushindi wakati matokeo yakiwa sare ya bao 1-1 na kuipatia ubingwa klabu yake. Walimaliza msimu kwa ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya JKT Ruvu. Kipre Tcheche alifunga bao lake la 13 la msimu na kuwa mfungaji bora wa klabu, Joseph Kimwaga na Mcha kila mmoja alifunga mara moja.

' YOSSO WALIWABEBA '. Joseph Kimwaga, alifunga bao la ushindi wakati timu yake ya Azam ilipopata ushindi wa kushangaza dhidi ya waliokuwa watetezi wa taji, Yanga. Matokeo yakiwa sare ya magoli 2-2. Kimwaga kinda wa timu ya pili alimalizia pasi ya Kipre Tcheche katika dakika ya mwisho, mwezi septemba, mwaka uliopita.

KELVIN FRED, kinda wa timu ya Taifa ya Vijana, Ngongoro Heroes, na timu ya Taifa ya Tanzania, alifunga goli la kusawazisha dakika tano kabla ya kumalizika kwa mchezo dhidi ya Yanga, 19 machi na kuisaidia timu yake iliyokuwa pungufu kwa zaidi ya dakika 25 kupata sare ya bao 1-1 na kulinda uongozi wao wa pointi saba dhidi ya Yanga. Michezo hii miwili ndiyo
iliyoamua bingwa, na Azam walifanikiwa kupata pointi nne dhidi ya Yanga, ambao waliifunga Azam katika michezo yote miwili msimu uliopita wakati walipotwaa ubingwa.


 Pointi sita walizopata Azam dhidi ya Simba zimekuwa changamoto kubwa kwa Yanga ambao wameshindwa kuwafunga mahasimu wao hao msimu huu. Kupata pointi kumi dhidi ya Simba na Yanga, na nyingine nne dhidi ya Mbeya City. kumewasaidia sana timu hiyo iliyoanzishwa mwaka 2007.

 KOCHA, OMOG... Akiwa tayari mshindi wa taji la kombe la Shirikisho Afrika, kocha Mcameroon, Patrick Omog alitua, Azam akitokea kwa mabingwa wa Congo Brazzaville, AFC Leopard. Ameiongoza. Azam katika michezo 14 hadi sasa. Amepoteza mchezo mmoja tu, wakati Azam ilipofungwa na kutolewa na Ferreviaro Beira ya Msumbiji katika kombe la Shirikisho, ameiongoza timu yake kupata ushindi mara 11, huku mara kumi akifanya hivyo katika ligi kuu Tanzania Bara. Azam chini ya Omog imetoa sare mara mbili tu katika michezo 13  ya mzunguko wa pili katika ligi kuu.

KUFUNGA MABAO NA KUZUHIA. Azam ilfunga magoli 53 na kuruhusu mabao 15 tu katika michezo 26 waliyocheza msimu uliopita. Azam walikuwa na ngome imara, viungo wazuri, na washambuliaji wakali kwa msimu mzima. Ukitoa timu ya Yanga ambayo imefunga magoli 59, magoli nane zaidi ya Azam walikuwa tiimu liyokamilika kila idara.

Timu ya mwisho nje ya klabu za Yanga na Simba ni Mtibwa Sugar ya Morogoro. Mtibwa walitwaa mfululizo ubingwa huo katika miaka ya 1999, na 2000. Timu nyingine ziliwahi kutwaa ubingwa wa ligi kuu Tanzania Bara, ni Coastal Union ya Tanga, 1988, Tukuyu Stars ya Mbeya, 1986, Pan Africans ya Dar es Salaam, 1982, Mseto ya Morogoro, 1975, na Cosmopolitan ya DAr es Salaam, 1967. Yanga SC, wametwaa ubingwa mara 24, Simba mara 19. Mtibwa mara mbili, na timu nyingine zimetwaa mara moja moja. Hongera AZam kwa kuwa mabingwa wapya wa ligi kuu Tanzania
Bara.

0714 08 43 98


Chanzo:shaffihdauda.com

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video