Thursday, July 31, 2014

Neymar reveals return date
Imechapishwa Julai 31, 2014, saa 9:23 alasiri

NEYMAR ameweka wazi kuwa atarudi uwanjani agosti 18 mwaka huu kuitumikia Barcelona katika mechi ya maandalizi ya kabla ya msimu ya kombe la Joan Gamper dhidi ya Leon.

Mbrazil huyo alivunjika mfupa wa uti wa mgongo wakati wa mechi ya robo fainali ya kombe la dunia dhidi ya Colombia na alizikosa mechi mbili.

Neymar aliwakosa Ujerumani, hatua ya nusu fainali na Uholanzi mechi ya mshindi wa tatu.

Hata hivyo anatarajia kujiunga na Barcelona katika maandalizi ya msimu Agosti 5 mwaka huu na ataweza kucheza kwenye mechi ya Gamper ndani ya dimba la Camp Nou.

“Naimarika taratibu kutokana na majeruhi. Nitarudi Barcelona kwa asilimia 100,” aliwaambia waandishi wa habari nchini Brazil.

“Nahitaji kuwa na msimu mzuri na naangalia mbele kuwasaidia wachezaji wenzangu kupata matokeo mazuri. Pia nahitaji kuisaidia timu ya Brazil.


“Nina imani ya kucheza mechi ya Gamper Agosti 18.” 

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video