- Edinson Cavan aliifungia Uruguay bao la kuongoza kwa njia ya mkwaju wa penati.
- Joel Campbell, Oscar Duarte na Marcos Urena waliifungia Costa Rica mabao yaliyowapa ushindi wa 3-1
- Luis Suarez alikaa benchi, lakini hakutumika katika mchezo wa wa usiku huu.
Kitu kambani: Edinson Cavani akiifungia Uruguay bao la kuongoza kwa njia ya penati na kushangilia kwa nguvu (pichani chini)
Cavani akishangilia penati aliyofunga.
Matokeo ya mechi hii ya
ufunguzi wa kundi D yanawapa nguvu England kufuzu katika kundi lao kama
watapata matokeo usiku huu dhidi ya Italia.
Cavani
aliifungia Uruguay bao la kuongoza kwa njia ya penati ya utata katika
dakika ya 21, lakini haikuweza kuwasaidia kuipuka kipigo.
Hata
hivyo kadi nyekundu ya kwanza katika fainali za kombe la dunia mwaka
huu imetokea baada ya beki wa kulia wa Uruguay, Maxi Pereira kumpiga
teke Campbell karibu na eneo la kona, hivyo mwamuzi wa mechi kuamua
kumtoa nje ya uwanja dakika za lala salama.
Mshambuliaji
wa Liverpool, Luis Suarez alianzia benchi na kumalizia mechi benchi
yaani hakucheza kabisa licha ya kuwepo kwenye orodha ya wachezaji wa
akiba, na hii inatokana na kushinda kuimarika ipasavyo kutoka kwenye
majeruhi ya goti alilofanyiwa upasuaji.
Ndosi kali: Oscar Duarte (kushoto) alifunga bao la pili na kuufanya ubao usomeke 2-1 kwa Costa Rica kabla ya kushangilia (chini, kushoto)
Oscar Duarte
0 comments:
Post a Comment