Friday, June 13, 2014

1

 Nahodha wa Yanga sc na timu ya taifa ya Tanzania, Taifa stars, Nadir Haroub `Cannavaro` mwenye jezi namba 13 wakati Stars ilipolazimisha sare ya 2-2 na Zimbabwe mjini Harare.

Na Baraka Mpenja, Dar es salaam

Imechapishwa Juni 13, 2014, saa 11:59 jioni

KIKOSI cha timu yoyote kinapoingia uwanjani, lazima awepo kiongozi ambaye hujulikana kwa jina la nahodha.
Nahodha katika timu ni mchezaji anayechaguliwa ndani ya kikosi kuwa kiongozi wa timu uwanjani: mara nyingi anakuwa mchezaji mkongwe au mwenye uzoefu kwenye kikosi au mchezaji mwenye ushawishi kwa wenzake. Nahadho wa timu anafahamika kwa kuvaa kitambaa kwenye mkono wake.
Hata timu ya taifa lazima iwe na nahodha wake kama ilivyo kwa Nadir Haroub `Cannavaro` ambaye anaiongoza Yanga na Taifa Stars.
Kibongo bongo, nahodha anaonekana mtu wa kawaida, huku baadhi ya makocha, viongozi na wachezaji wengine wakimchukulia mtu wa kawaida, lakini kwa wenzetu, unahodha ni cheo kikubwa sana.
Nahodha ni mtu mwenye ushawishi hata kwa kocha wa timu. Wachezaji wanamheshimu kwa nafasi yake na kumsikiliza kila anapozungumza.
Majukumu rasmi ya nahodha yanayotambuliwa na sheria za mchezo ni kushiriki kwenye zoezi la urushaji wa shilingi wakati wa kuchagua magoli pindi mechi inapotaka kuanza na huwa wa kwanza kupiga penati.
Kinyuma na wengi wanavyofikiri, kisheria nahodha hana mamlaka ya kupinga maamuzi ya mwamuzi. Japokuwa mwamuzi anaweza kuzungumza na nahodha wa timu yoyote kuhusu tatizo la mchezo pale inapobidi.
 ccc
Nahodha wa Azam fc, John Raphael Bocco `Adebayor` wa kwanza kulia akiwa ameshikilia kombe la ligi kuu walilotwaa msimu uliopita

Kuna wakati ukienda mitaani kuangalia ndondo, nahodha anaweza kumkomalia mwamuzi bila kujua hana uwezo huo.
Hii inatokana na watu kutojua wajibu wa nahodha uwanjani, lakini kupitia makala hii maalum kwa kutoa elimu, kazi za mtu huyu zitafahamika.
Wakati wa zoezi la ugawaji wa zawadi kwenye mechi inayoipa ubingwa timu fulani, nahodha ndiye anawaongoza wachezaji wenzake kuvalishwa medali. Kombe ambalo timu imeshinda, nahodha ndiye wa kwanza kukabidhiwa na ndiye atakuwa wa kwanza kulinyanyua juu.
Nahodha ndiye mwenye kazi kubwa ya kupandisha morali ya wachezaji inaposhuka, yeye ndiye mwenye majukumu ya kuwaunganisha wenzake ili wafanye kazi nzuri wawapo uwanjani.
Nahodha anaweza kuungana na kocha kwenye uteuzi wa kikosi cha kwanza kwa baadhi ya mechi. Kwenye michezo ya vijana au michezo ya kawaida ya kujiburudisha, mara nyingi nahodha anakabidhiwa majukumu makubwa ambayo yanatakiwa kufanywa na kocha.
 http://1.bp.blogspot.com/-NGXkoERvGZE/UxJKpVoROfI/AAAAAAAADVA/EqD9ReOUEI4/s1600/Yanga.jpg
Nahodha siku zote huwa anakuwa kiungo au beki na mara chache anaweza anaweza kuwa mlinda mlango au mshambuliaji, na hii inatokana na sehemu wanazokaa wachezaji hawa na majukumu yao mazito uwanjani.
Nahodha wa klabu anateuliwa kwa msimu. Kama hayupo au hajachaguliwa kwa ajili ya mchezo fulani, nahodha msaidizi ndiye atateuliwa kufanya majukumu yake.
Nahodha wa mechi ndiye mtu wa kwanza kubeba kombe ambalo timu imeshinda hata kama sio nahodha wa klabu. Mfano mzuri ni UEFA ya mwaka 1999 wakati nahodha wa mechi Peter Schmeichel alinyanyua kombe la Manchester United kwasababu nahodha Roy Keane alikuwa amesimamishwa.
Mwaka 2012 kwenye michuano ya UEFA, nahodha wa mechi (ambaye alikuwa nahodha msaidizi) Frank James Lampard kwa pamoja walinyanyua kombe na John Terry aliyekuwa anatumikia adhabu, lakini alipewa ruhusa maalum na UEFA.
Nahodha msaidizi ni mchezaji anayetarajia kuiongoza timu wakati nahodha hajapangwa kwenye kikosi cha kwanza au amekwenda benchi na kumpisha mchezaji mwingine au amepata kadi nyekundu.
Mara nyingi nahodha msaidizi huwa anateuliwa kuwa nahodha mkuu pale nahodha anapoondoka katika klabu, mfano Iker Casillas alimbadili Raul Gonzalez katika klabu ya Real Madrid.
Kwa kifupi huyu ndiye nahodha ambaye anatakiwa kuheshimika na kuwa na uwezo mkubwa uwanjani na utashi wa kuongoza wenzake.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video