Tuesday, June 10, 2014



 http://3.bp.blogspot.com/-dKHmZYKCSvE/UzrovYg6pAI/AAAAAAAAK9Y/Rqex7gFN-as/s1600/RUVU+Shooting+Stars.jpg
Na Baraka Mpenja, Dar es salaam

Imechapishwa Juni 10, 2014, saa 4:56 asubuhi

MAAFANDE  wa Ruvu Shooting wamedhamiria kufanya maajabu katika msimu wa 2014/2015 wa ligi kuu soka Tanzania bara unaotarajia kuanza kutimua vumbi mwezi agosti mwaka huu.
Masau Bwire, afisa habari wa klabu hiyo ameuambia mtandao huu kuwa wanaendelea vizuri na mazoezi waliyoanza jana chini ya kocha mkenya, Tom Alex Olaba katika uwanja wao wa Mabatini, Mlandizi, mkoani Pwani.
Masau amesema nia yao ni kujiimarisha mapema ili kuleta changamoto mpya na ili kufanikisha ndoto hiyo, ndio maana Shooting imekuwa timu ya kwanza kuingia kambini.
“Lengo letu ni kuchukua ubingwa au nafasi ya pili. Tukishindwa sana, sana tunahitaji nafasi ya tatu. Hatuongei kwa kujifurahisha, tunajipanga vilivyo”. Amesema Masau.
Afisa habari huyo alisema bado kurunzi zao zinaangaza huku  na kule illi kupata nyota wengine watakaokuwa msaada mkubwa kwa msimu ujao.
Masau alisema Olaba aliagiza wapatikane wachezaji wenye uzoefu na ligi kuu na kwa kutekeleza hilo wamesajili wachezaji kadhaa akiwemo beki wa kati wa Mtibwa Sugar, Salvatory Ntebe.
“Hatujamaliza usajili, bado kurunzi yetu inaangaza huku na kule. Tumedhamiria kufanya makubwa sana msimu ujao”. Alisema Masau.
Katika hatua nyingine, Masau alisema Ruvu Shooting ni klabu inayowajali wachezaji wake nje na ndani ya uwanja.
“Kuna taarifa mbaya kwetu sisi. Kuna wachezaji tumevunja mikataba yao na wanatusema vibaya. Lakini nikwambie, moja ya timu inayojali wachezaji hapa Tanzania, Ruvu shooting ni kiboko”. Alisema Masau.
Hivi karibuni mchezaji wa klabu hiyo, Cosmas Adel Lewis alivunja mkataba na klabu hiyo na kudai kuwa hakuridhishwa na maisha ya Mabatini.
Cosmas alisema mpira ni ajira yake na anautumia kujiingizia kipato, lakini kwa mazingira ya Shooting asingetimiza malengo yake ikizingatiwa yeye bado ni kijana mdogo.
Nyota huyo aliuponda uongozi wa klabu hiyo kwa kushindwa kuwajali wachezaji wake kimaslahi na ikafikia wakati wanatoroka kambini kwenda kucheza ndondo ili kujiongezea kipato.
Akijibu hilo, Masau alisema mchezaji kutoroka kambini na kwenda kucheza ndondo ili kujiongezea kipato halikubaliki hata kidogo na kama aliona pesa haimtosha, kwanini alisaini mkataba?.
Masau alisema wachezaji walioachana na klabu hiyo waache kuipaka matope kwenye vyombo vya habari.
Cosmas alisema kuna timu za ligi kuu amekwishazungumza nazo, na wakati wowote atasaini mkataba na moja ya klabu ya ligi kuu.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video