LICHA ya kukosekana kwa mshambuliaji wao nyota Radamel Falcao, Colombia wameanza vizuri kombe la dunia baada ya beki wa kulia wa Napoli, Pablo Armero kuwafungia bao la kuongoza katika dakika ya 5 dhidi ya Ugiriki.
Shuti la Armero halikuwa kali kuliko tuliyoyaona siku tatu za ufunguzi, lakini staili yake ya kucheza akishangilia bao lake mbele ya benchi la Colombia ilikuwa nzuri na bora mpaka sasa, labda ndio inaweza kuwa kali zaidi katika mashindano ya mwaka huu.
Sukuma: Armero akiwaonesha wachezaji wenzake sehemu ya kwenda kabla ya kuanza kucheza akishangilia bao lake .
Twende kazi: Wachezaji wa Colombia wakijiandaa kuanza kucheza kwa mpangilio wakishangilia bao.
Pamoja: Wachezaji wa Colombia wakishangilia kwa pamoja baada ya bao la Armero lililowafanya wawe mbele katika dakika ya tano.
Mikono juu: Colombia wameanza vizuri katika kundi lao la C baada ya kuifunga Ugiriki
0 comments:
Post a Comment