Tuesday, June 10, 2014



 http://www.mwananchi.co.tz/image/view/-/2330772/highRes/754518/-/maxw/600/-/eoxv0t/-/wambura.jpg
Na Baraka Mpenja, Dar es salaam

Imechapishwa Juni 10, 2014, saa 1:40 usiku

MUDA wowote kutoka sasa bomu la Michael Richard Wambura linaweza kulipuka baada ya taarifa za ndani kueleza kuwa mvutano umekuwa mkali baina ya wajumbe wa kamati ya rufani ya shirikisho la soka Tanzania, TFF juu ya kurudi au kuondolewa kwa mgombea huyo katika nafasi ya urais kwenye uchaguzi wa Simba unaotarajia kufanyika juni 29 mwaka huu.
Wambura alikata rufani kupinga maamuzi ya kamati ya uchaguzi ya Simba chini ya mwenyekiti wake, Wakili, Damas Ndumbaro akipinga kuenguliwa kwenye mchakato wa uchaguzi.
Mgombea huyo aliondolewa kwasababu kubwa mbili, moja ni kuipeleka Simba mahakamani na pili ni kusimamishwa uanachama wake.
Mtandao huu upo maeneo ya tukio kufuatilia `ngado kwa ngado` na mara taarifa rasmi itakapotoka, itatolewa kwa wadau wote.
Kumekuwepo na taarifa nyingi zinasambazwa na watu mbalimbali kuwa Wambura anarudi na wengine wanasema anaondolewa, lakini ukweli ni kwamba taarifa rasmi kutoka ndani ya Hotel ya Courtyard, Upanga, jijini Dar es es salaam, haijatoka.
Zoezi lilioanza mchana wa leo ni kuyapitia maelezo ya pande zote na mpaka muda huu bado maamuzi hayajawekwa hadharani na wajumbe bado wapo ndani ya ukumbi.
Ngoma ya Wambura inaonekana nzito, lakini mwisho wa siku lazima maamuzi yafikiwe.
Endelea kuwa nasi na tutawapeni taarifa rasmi muda wowote zitakapotoka, ingawa kuna taarifa za chini ya kapeti kuwa Wambura anarudi.
Taarifa hizi si rasmi, hivyo zinaweza kuwa sahihi au zisiwe sahihi kwasababu bado kuna usiri mkubwa kutoka ndani ya ukumbi.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video