Uchaguzi wapigwa pini: Rais wa TFF, Jamal Malinzi ametangaza kusimamisha uchaguzi wa Simba sc
Na Baraka Mpenja, Dar es salaam
Imechapishwa Juni 15, 2014, saa 8:00 mchana
RAIS wa shirikisho la soka Tanzania, TFF, Jamal Emil Malinzi, jana aliwaalika waandishi wa habari akiwaomba wafike leo mchana majira ya saa 6:00 katika ofisi za shirikisho hilo kwa lengo la kutoa ujumbe kwa umma wa wapenda michezo Tanzania.
Wengi hawakupata majibu juu ya nini Rais Malinzi
anataka kuzungumza na wanahabari kwasababu si kawaida yake kufanya mikutano na
waandishi mara kwa mara.
Akitokea Brazil kwenye mkutano wa 64 wa FIFA hivi
karibuni, hatimaye mchana wa leo, Rais Malinzi amekutana na waandishi wa habari
katika ukumbi wa mikutano wa shirikisho hilo, uliopo makao makuu katikakati ya
jiji la Dar es salaam na kutangaza kusimamisha mchakato wa uchaguzi wa klabu ya
Simba ulioatarajia kufanyika juni 29 mwaka huu hadi hapo itakapounda kamati ya
Maadili itakayokuwa na jukumu la kusikiliza masuala ya maadili kuelekeza
uchaguzi huo.
Rais Malinzi amesema Simba inatakiwa kukamilisha
zoezi hilo la kuunda kamati ya Maadili hadi kufikia juni 30 mwaka huu ili
mchakato wa uchaguzi uweze kuendelea chini ya mwenyekiti wa kamati ya uchaguzi,
wakili, Dkt. Damas Daniel Ndumbaro.
Mpiganaji: Rais wa Simba sc, Ismail Aden Rage ataendelea kuiongoza klabu hiyo.
Wengi walijiuliza kwanini TFF imefikia uamuzi huo,
lakini Malinzi alifafanua kuwa hatua hiyo imekuja kufuatia kuibuka kwa
malalamiko mengi ya kimaadili, hivyo kamati hiyo itayasikiliza na kufikia
maamuzi.
Uchaguzi wa Simba uliopangwa kufanyika juni 29
mwaka huu uliingia sura mpya tangu Michael Richard Wambura aliopoenguliwa
kugombea nafasi ya Urais.
Suala hilo lilionekana kugusa watu wengi, lakini
alipokata rufani na kushinda, mengi yakaibuka zaidi na baadhi ya wanachama
walipinga kurudishwa kwake katika uchaguzi wa Simba.
Hata hivyo, Malinzi amekiri kuwa TFF imepokea
malalamiko mengi juu ya ukiukwaji wa maadili kwa baadhi ya wagombea na
wanachama wa klabu hiyo, hivyo ni muhimu kuundwa kwa kamati ya maadili itakayoshughulikia
mambo hayo.
Wakati huu ambapo kamati itakuwa ikiundwa, kamati
ya utendaji ya Simba iliyopo madarakani kwasasa, chini ya Rais wake, Ismail
Aden Rage itaendelea kuiongoza klabu hiyo hadi hapo mchakato wa uchaguzi
utakapokamilika.
Jana Rage wakati anazungumza na mtandao huu
alisema anajitahidi kuhakikisha anaacha mchoro au msingi au hata ghorofa moja
ya Hosteti za wachezaji katika eneo lake la Bunju ili kuepukana na gharama
kubwa wanazotumia kuwaweka wachezaji hotelini wanapofanya kambi.
Rage aliyasema hayo kufuatia uongozi wake kuanza
utekelezaji wa ujenzi wa uwanja wa kisasa ambapo tayari magereda na malori
yalishapelekwa kwajili ya kazi.
0 comments:
Post a Comment