Sunday, June 15, 2014



http://shaffihdauda.com/wp-content/uploads/2014/04/MKWASA.jpg
Unapiga hivi! sawa?: kocha msaidizi wa Yanga, Charles Mkwasa akiwaelekeza wachezaji wake kwenye moja ya mazoezi ya timu hiyo  msimu uliopita.

Na Baraka Mpenja, Dar es salaam
0712461976

Imechapishwa Juni 15, 2014 saa 8: 31 mchana

KOCHA  msaidizi wa klabu ya Dar Young Africans, Charles Boniface  Mkwasa `Master` amewashauri wachezaji wa Tanzania kutumia michuano ya kombe la dunia inayoendelea nchini Brazil kama sehemu ya darasa la kupata vitu vipya.
Mkwasa amezungumza na MPENJA BLOG mchana huu na kueleza kuwa kombe la dunia ni michuano inayowakutanisha  wachezaji wa aina zote, wakongwe na vijana, hivyo wachezaji wa Tanzania wanatakiwa kutumia muda kuwaangalia na  kujifunza na si kujifurahisha.
“Wachezaji wanaochezaji kombe la dunia wengi ni `maproo`. Wana vitu vingi kuliko wachezaji wetu. Sisemi wajifunze wawe kama wao, lakini angalau  watoke na vitu vichache vinavyoweza kuwasaidia katika maisha yao ya soka”. Alisema Mkwasa.
Mkwasa aliongeza kuwa kujifunza kwa kumtazama mtu aliyekuzidi ni jambo jema kwasababu unaona vitu ambavyo hujawahi kufanya na hivyo kuwa katika nafasi nzuri ya kujaribu kuvifanyia kazi.
Akizungumzia fainali za mwaka huu za kombe la dunia, Mkwasa alisema alichokiona mwaka huu ni mchanganyiko mkubwa wa wachezaji.
“Timu nyingi zimewapa nafasi chipukizi na wanafanya kazi nzuri. Angalia timu kama Costa Rica, wana vijana wadogo ambao ni hatari sana. Fundisho kubwa kwetu ni kuwaamini vijana na kuwapa nafasi”. Alisema Mkwasa.
Kuhusu Hispania, Mkwasa alisema wana nafasi ya kufanya vizuri katika mechi mbili walizonazo, lakini akaonya kuwa kama watajiamini wanaweza kutolewa mapema.
“Wamefungwa mabao 5-1 na Uholanzi. Nilichokiona mimi ni kwamba waliingia kwa kujiamini sana, na kadri walivyofungwa zaidi, walizidi kujichanganya”. Aliongeza Mkwasa.
Mkwasa kwasasa anasubiri klabu yake ya Yanga ipate  kocha mkuu atakayefanya kazi naye katika msimu wa 2014/2015 wa ligi kuu soka Tanzania bara, ingawa bado haijawekwa wazi kama ataendelea na kibarua hicho.
Mwenyekiti wa Yanga, Yusuf Manji yupo katika mazungumzo na kocha wa zamani wa timu ya Taifa ya Tanzania, Taifa stars, Mbrazil Marcio Maximo, na kuna taarifa kuwa mazungumzo hayo yamefikia hatua nzuri.
Mara wakapomalizana, Maximo atatua nchini na kuanza rasmi kukinoa kikosi cha Yanga, lakini haijulikani kama Mkwasa ataendelea kuwa msaidizi wa kocha mpya.
Mkwasa alikuwa msaidizi wa kocha  Hans Van der Pluijm msimu uliopita, lakini Mholanzi huyo alitimkia Uarabuni baada ya kumaliza mkataba wake wa miezi sita jangwani.
Maximo atakapokuja nchini, mpinzani wake mkuu atakuwa kocha mkuu wa Simba sc, Mcroatia Dravko Logarusic aliyeongezewa mkataba wa miaka miwili na klabu ya Simba kufuatia ule wa kwanza wa miezi sita kumalizika.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video