Friday, June 13, 2014



 
Imechapishwa Juni 13, 2014 saa 7:08 mchana

BAADA ya Simba kumkosa kipa wa Yanga, Ally Mustapha ‘Barthez’ ambaye amesaini mkataba mpya na timu yake, kocha wa makipa wa Msimbazi, Iddi Pazi, amesema hakuna jinsi, haraka sana Juma Kaseja anatakiwa kurudi Simba ili acheze kwa raha.
Kabla ya Yanga kumsainisha Barthez, Simba ilikuwa imepiga hesabu za kumrudisha kipa wao huyo wa zamani ili apambane na Ivo Mapunda ambaye hana mpinzani katika kikosi cha timu hiyo.
Kocha huyo alisema, kuna sababu tatu zinazomfanya Kaseja kuondoka Yanga kwani akibaki hatoweza kufanya kazi yake kwa furaha na mafanikio.
Alisema kwanza ushindani wa nafasi kati yake na makipa Deo Munishi ‘Dida’ na Barthez ni mkubwa. Pili anaonekana hakubaliki kwa mashabiki wa Yanga na tatu ni ujio wa kocha Marcio Maximo katika kikosi hicho.
Pazi alisema: “Mahali alipo Kaseja (Yanga), kunaweza kumfanya astaafu kabla ya muda wake au hata kuendelea kucheza soka kwa mashaka hivyo namtaka afikirie kurudi Simba ili kutunza heshima na kufanya kazi yake kama ilivyokuwa awali.
“Kaseja si kipenzi cha mashabiki Yanga na inapokuja wakati wa kazi anaweza kupata wakati mgumu kutokana na kuzomewa na kumfanya kutojiamini akiwa kwenye kazi yake.
“Pia nimesikia Yanga wanamleta Maximo, nafikiri ni hofu kwa Kaseja kwa sababu siku za nyuma kocha huyo alitofautiana naye wakiwa Taifa Stars, aje Simba ili awe na amani.”
Pazi pia amemtaka kipa huyo kufuta ndoto za kustaafu soka wakati huu ili awe kocha akisema kipa huyo bado ana uwezo wa kucheza.
“Nafikiri wapenzi wa Simba wanatakiwa kumpa Kaseja nafasi kwenye mioyo yao. Amefanya mengi na naamini akirudi ataweza kufanya mengi na kumalizia soka lake Simba akiwa na heshima,” alisisitiza.

CHANZO: MWANASPOTI

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video