Tuesday, June 10, 2014


http://ptblog.pesatimes.com/wp-content/uploads/2014/04/DSCN1347-FILEminimizer.jpg
Tom Alex Olaba ameanza kunoa kikosi chake mapema ili kufuata mbio za Mbeya City FC waliozitikisha Simba, Yanga na Azam fc msimu uliopita.

 Na Frank Momanyi, Dar es salaam

Imechapishwa Juni 10, 2014, saa 6:17 mchana

KLABU ya Maafande wa Ruvu Shooting yenye maskani yake Mabatini mkoani pwani imeingia kambini rasmi tayari kwa kujiwinda na mikikimikiki ya ligi kuu soka Tanzania bara msimu mwaka 2014-2015 unaotarajia kuanza kushika kasi agosti mwaka huu.
Akizungumza na MPENJA BLOG , msemaji wa maafande hao, Masau Bwire amesema wameanza kambi hiyo mapema kwa ajili ya kujiweka fiti kwa msimu ujao, huku lengo hasa likiwa ni kupata pointi tatu muhimu kwa katika kila mchezo wa ligi kuu.
Masau alisema tayari wamenasa baadhi ya wachezaji nyota hapa nchini kutoka katika  klabu kama vile Mtibwa sugar pamoja na kagera sugar watakaokisaidia kikosi hicho baada ya kuvurunda msimu uliopita na kumaliza katika nafasi ya sita ya msimamo wa ligi.
“Tumeamua kuanza maandalizi kabambe ya kujiandaa na ligi msimu ujao, na sio maandalizi  ya zima moto,  bali ni maandalizi ya nguvu yatakayoleta mafanikio katika klabu yetu”.
“Kocha Alex Olaba yupo katika hali nzuri ya kukiimarisha kikosi, na ndio maana tumeingia kambini mapema zaidi kuliko klabu zingine hapa nchini.
“Lengo hasa likiwa ni kutimiza ndoto zetu za kutwaa ubingwa wa ligi kuu soka Tanzania bara msimu ujao”alisema Masau.
http://www.fullshangweblog.com/wp-content/uploads/2014/03/237.jpg
Ruvu Shooting hawataki tena kupigwa 7-0 na Yanga, ili kukwepa kipondo, haoooo! kambini jana
 Msimu uliopita, Maafande wa Ruvu Shooting walifanikiwa kumaliza katika nafasi ya sita ya msimamo katika ligi ambayo ilikuwa na upinzani wa aina yake kutoka kwa klabu kama vile Mbeya City ambayo ilipanda daraja na kuleta changamoto kubwa na kumaliza mzunguko wa kwanza bila kupoteza mchezo hata mmoja.
Ruvu Shooting katika michezo 26 ya msimu uliopita, walifanikiwa kujikusanyia pointi 38 ambapo walishinda mechi 10, sare 8 na kufungwa mechi 8.
Walifunga magoli 28 na kuruhusu nyavu zao kuguswa mara 38, hivyo wastani wa mabao ya kufunga na kufungwa yalikuwa hasi nne (-4).
Wapiga kwata hao wanaona matokeo hayo yalikuwa mabaya kwao, hivyo hatua ya kwanza ya kuyafuta msimu ujao na kuandika matokeo mazuri zaidi ni kuingia kambini kuanza maandalizi ya mapema.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video