Tuesday, June 10, 2014


http://2.bp.blogspot.com/-4GFz77Ybc5M/Uozo-zA6MiI/AAAAAAAAn3I/gtuS_lVfzAY/s1600/kapombe+3.jpg
Kapombe akiwa Ufaransa kabla ya kurejea nchini

Na Baraka Mpenja, Dar es salaam

Imechapishwa Juni 10, 2014, saa 3:13 usiku

SHOMARY Kapombe amesema ubora wa wachezaji na makocha wa mabingwa wa ligi kuu soka Tanzania bara,  Azam fc ndio sababu kubwa yeye kuchagua kujiunga na klabu hiyo kuelekea msimu mpya wa ligi kuu unaotarajia kuanza kushika kasi mwezi Agosti mwaka huu.
Siku za karibuni, beki huyo kiraka aliamua kusaini mkataba wa miaka mitatu Azam fc na ataitumikia klabu hiyo msimu ujao wa ligi kuu na michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika.
Kapombe alisema kucheza Azam fc kwasasa ni salama kuliko klabu yoyote ya Tanzania kwani wanalipa vizuri na wanawajali wachezaji kwa kila kitu.
Aliongeza kuwa Azam imejikamilisha kwa kila kitu kuanzia uwanja na vifaa vya mazoezi.
Aidha Kapombe alisema yeye anapenda ushindani katika soka, hivyo anapenda kucheza  timu yenye wachezaji wakali.
“Azam kuna ushindani mkubwa. Binafsi sipendi kucheza timu isiyo na ushindani. Kama kuna ushindani, kunanifanya nifanye mazoezi sana”. Alisema Kapombe.
Pia alikiri kujawa na furaha baada ya kurudi nyumbani na hususani klabu bora ya Azam fc na anaamini timu hiyo itarudisha makali yake.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video