Wednesday, June 11, 2014



 http://4.bp.blogspot.com/-Oo1XoUo9UHQ/UPVjccFbvYI/AAAAAAAAUiw/mYHH6NJ0_UY/s1600/DSC05070.JPG
Tabasamu tu: Michael Richard Wambura amemfunga bao tamu mwanasheria Dkt. Damas Ndumbaro baada ya kamati ya Rufani ya TFF kumrudisha, sasa vita ni kati yake na  Evanc Aveva kwenye king`anyiro cha Urais katika uchaguzi wa juni 29 mwaka huu.

Na Baraka Mpenja, Dar es salaam

Imechapishwa Juni 11, 2014, saa 11:05 jioni

SAA chache baada ya kamati ya Rufani ya shirikisho la kandanda Tanzania, TFF, chini ya mwenyekiti wake, Wakili Julius Mutabazi Lugaziya kumrudisha, Michael Richard Wambura kwenye uchaguzi wa Simba sc, mgombea huyo amesema sasa haki imetendeka na uchaguzi utakuwa wa amani.
Wambura amezungumza na mtandao huu dakika chache zilizopita na kusema kuwa anaufananisha ushindi wake kama mchezo wa mpira wa miguu.
“Mpira wa miguu una mechi ya nyumbani na ugenini,  unaweza ukafungwa ugenini, ukashinda nyumbani, bila kujali umeshinda goli ngapi, lakini ninachoweza kusema ni kwamba haki imetendeke, matokeo yametoka, tujipange kwenda kwenye uchaguzi ili wanasimba wapate viongozi wao wanaowataka”. Amesema Wambura.
Mgombea huyo ameongeza kuwa hiki sio kipindi tena cha kutafuta mchawi, bali ni kipindi kinachohitaji wanasimba kuwa makini.
“Ni kipindi cha kuwa makini, kuweka sera zetu hadharani, malengo yetu hadharani, ili wana Simba wapate fursa ya kuchagua kwa sera, nadhani hilo ndio ombi langu”. Ameongeza Wambura.
Hata hivyo, Wambura amesema kesho ataongea na waandishi wa habari makao makuu ya klabu ya Simba mtaa wa Msimbazi, kariakoo jijini Dar es salaam.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video