Nimewaua!: Mshambuliaji wa Yanga sc, Jerryson Tegete ( wa kwanza kushoto) akishangilia moja ya bao lake msimu uliopita na wachezaji wenzake, Mrisho Ngassa (katikati) na Saimon Msuva (kulia).
Na Baraka Mpenja, Dar es salaam
Imechapishwa Juni 15, 2014, saa 8:40 mchana
MSHAMBULIAJI wa Yanga sc, Jerryson John Tegete
amefurahishwa na viwango vya timu zinazoshiriki kombe la dunia mwaka huu nchini
Brazil japokuwa bado michuano ni mibichi kabisa.
Tegete amezungumza na MPENJA BLOG mchana huu na kueleza kuwa Cameroon ilianza kwa
kufungwa na Mexico bao 1-0, lakini walikuwa na nafasi ya kufanya vizuri.
“Timu za Afrika zimejiandaa vizuri. Cameroon wangekuwa
makini wangefaya vizuri”. Alisema Tegete.
“Nimewaona Ivory costa wakicheza, sio wabaya, kuna
makosa machache wanafanya na wanapoteza nafasi nyingi, lakini nadhani
wawakilishi wa Afrika watafanya vizuri tu”.
Tegete aliongeza kuwa kitu alichojifunza kwa mechi
hizi za mwanzo ni timu kucheza kitimu zaidi na si mchezaji mmoja mmoja, jambo
ambalo amelipenda na angetamani wachezaji wenzake wajifunze.
Pia amekiri kuw ajuzi hauzeeki baada ya kiungo
mkongwe wa Italia, Andrea Pirlo kuonesha kandanda safi kwenye mchezo dhidi ya
England.
“Nimefurahishwa sana na kiwango cha Pirlo katika,
unaona alivyocheza vizuri jana, hili ni fundisho kuwa ukiwa na nidhamu ya
mpira, utaucheza kwa muda mrefu”.
Pirlo amezidi kuonesha utaalam wake licha ya umri kumuacha
“Pia bao la Van Persie nimelipenda sana. Alifunga wakati muafaka, alijituma na kuisaidia Uholanzi. Aliuvaa unahodha wake. Ni fundisho zuri kwangu”. Alisema Tegete.
“Pia bao la Van Persie nimelipenda sana. Alifunga wakati muafaka, alijituma na kuisaidia Uholanzi. Aliuvaa unahodha wake. Ni fundisho zuri kwangu”. Alisema Tegete.
Pia nyota huyo wa Yanga alisema wachezaji vijana
kama Neymar wameleta changamoto kubwa katika mashindano na kuyafanya yawe na
mvuto.
Tegete ni moja ya washambuliaji walioibuliwa na
Maximo akiwa kocha wa Taifa stars, na kama kweli kocha huyo atarejea nchini,
basi Tegete anaweza kuzaliwa upya.
Kwa misimu miwili sasa, Tegete hajafanya vizuri
akiwa na klabu yake ya Yanga, lakini alikiri kuwa majeruhi ya goti yamemsumbua
kwa muda mrefu.
Mechi za mwishoni mwa msimu uliopita, Tegete
alirudi katika kiwango kizuri sambamba na mshambuliaji aliyesajiliwa na Yanga
kutokea klabu ya Mtibwa Sugar, Hussein Javu.
Tegete alisema kwakuwa amepona goti, msimu ujao
atafanya vizuri na mpaka kurejea timu ya taifa ya Tanzania, Taifa stars chini
ya kocha Mholanzi, Mart Nooij.
0 comments:
Post a Comment