Wednesday, June 11, 2014




 SAM_0369
Wamemrudisha Wambura: Wa kwanza kutoka kulia ni Mkurugenzi Msaidizi, Sheria na Wanachama TFF, Eliud Mvela, (Katikati) ni mwenyekiti wa kamati ya rufani ya TFF, Wakili, Julius Mutabazi Lugaziya na  ( watatu kutoka kushoto) ni Juma Abeid Spencer, mjumbe wa kamati ya rufani wakati wa mkutano na waandishi wa habari mchana huu.
 


Na Baraka Mpenja,  Dar es salaam

Imechapishwa Juni 11, 2014, saa 8:14 mchana

KAMATI ya rufani ya shirikisho la soka Tanzania,  TFF, imetengeu maamuzi ya kamati ya uchaguzi wa klabu ya Simba sc wa kuliengua jina  la mgombea wa Urais wa klabu hiyo, Micheal Richard Wambura.
Mwenyekiti wa kamati hiyo, wakili Julius Lugaziya amesema mchana huu katika mkutano na waandishi wa habari kwenye ukumbi wa mikutano wa TFF, jijini Dar es salaam kuwa kamati yake ilikaa juzi na jana na kufikia maamuzi ya kutengue maamuzi ya kamati ya uchaguzi ya Simba chini ya mwanasheria, Dkt. Damas Ndumbaro kwasababu klabu hiyo ilikiuka kanuni ilijiwekea yenyewe kwa mujibu wa katiba.
Lugaziya amesema kuwa uamuzi wa kumrudisha Wambura umeangali zaidi busara kwasababu Simba ilikiuka katiba yake kwa kumuacha mwanachama aliyesimamishwa kuendelea kufanya shughuli za klabu, na kama akiondolewa basi katiba na kamati ya uchaguzi vyote vitakuwa batili.
 “Tangu aliposimamishwa, muomba rufani (Wambura)  hajawahi kuchukuliwa kama mtu aliyesimamishwa. Kwanini?, kupoteza haki za uanachama ni pamoja na kupoteza haki za kulipa ada, haki za kushiriki mikutano, haki ya vikao vya maamuzi na haki ya kuteuliwa katika vyomvyo mbalimbali vya Simba SC”. Alisema Wakili Lugaziya.

“Tangu kutangazwa kusimamishwa, amekuwa akishiriki shughuli za Simba”
“Amekuwa akishiriki mikutano yote mikuu na dhararu, ikumbukwe kuwa mwanachama halali tu ndiye anatakiwa kushiriki mikutano hiyo na mwanachama ambaye amesimamishwa hatakiwi kushiriki, lakini tangu kutangaza kusimamishwa, Wambura amekuwa akishiriki”. Alifafanua Lugaziya.
“Kubwa zaidi, mpaka sasa Wambura ni mjumbe wa kuteuliwa wa kamati ya utendaji ya Simba na alishiriki katika mikutano ya katiba pamoja na kushiriki kuiteua kamati ya uchaguzi”.
 wambura


Moto kuwaka: Wambura dhidi ya Aveva ngoma nzito uchaguzi Simba sc, jamaa arudishwa na kamati ya rufani. 
 

Wakili huo aliongeza kuwa kama mtu batili ameshiriki kufanya maamuzi, basi maamuzi nayo ni batili.
“Wambura alishiriki katika mkutano wa katiba na kuiteua kamati ya uchaguzi, maana yake kama Wambura ni batili, basi katiba na kamati ni batili”.
“kama tunafikia maamuzi ya kusema katiba na kamati  ya uchaguzi ya Simba si halali, kwasababu mtu batili alishiriki,  athari yake ni kubwa. Kamati alishasema huko nyuma kwamba Simba ilikuwa inamchukulia Wambura kama mwanachama”. Alisema Lugaziya.
“Naomba mnielewe kuwa uamuzi huu, hauna maana nyingine au nia ya kutoa mlango kwa wanachama wa Simba au klabu nyingine kwenda mahakamani, bali ni kwamba unawataka wanachama wa TFF kuzingatia na kufuata taratibu walizojiwekea na si kutizumia kwa manufaa ya wachache katika mchezo wa mpira wa miguu”.
“Kamati ya uchaguzi ya TFF inabatilisha uamuzi wa kamati ya uchaguzi ya Simba. Michael Richard Wambura anastahili kugombea katika uchaguzi huo”. Alimaliza Wakili Lugaziya.
Hata hivyo, Lugaziya alifafanua kuwa uamuzi umefikiwa kwa wingi wa kura kwasababu maamuzi ya vikao kama hivyo kama wajumbe wanashindwa kufikia muafaka maamuzi yanaamuriwa kwa kupiga kura.
Hii ni mwanzo, yapo mengi yamezungumzwa na mtandao huu utakuletea habari zaidi. Endelea kuwa nasi.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video