Tuesday, June 10, 2014



 http://ptblog.pesatimes.com/wp-content/uploads/2014/05/wabura-33.jpg
Na Baraka Mpenja, Dar es salaam

0712461976

Imechapishwa Juni 10, 2014, saa 2:37 usiku

HATIMAYE  kamati ya rufani ya shirikisho la soka Tanzania, TFF imemaliza kujadili rufani ya mgombea wa urais katika uchaguzi wa klabu ya Simba sc unaotarajia kufanyika juni 29 mwaka huu, Michael Richard Wambura.
Kamati ya Rufani chini ya mwenyekiti wake,wakili,  Julius Luhaziya imekaa kuanzia jana juni 9 mpaka jioni ya leo (juni 10) katika Hoteli ya Courtyard iliyopo Upanga , jijini Dar es salaam.
Kikao hicho kilichojaa usiri mkubwa kimemalizika jioni ya leo na kufikia maamuzi juu ya rufani ya Wambura, lakini mwenyekiti wa kamati , Lugaziya ataongea na waandishi wa habari kesho mchana majira ya saa 6:00 katika ukumbi wa mikutano wa TFF.
Afisa habari wa shirikisho la soka Tanzania, TFF, Boniface Wambura Mgoyo dakika chache zilizopita amesema kuwa kamati imeshamliza na kufoloa maamuzi juu ya hatima ya Richard Wambura, lakini yeye hataki kuwa msemaji wake kwani mwenyekiti atakuwa na mkutano na waandishi wa habari hapo kesho mchana.
Wambura amefafanua kuwa kamati hiyo imekaa kwa siku mbili kwasababu ndio chombo cha kutenda haki kwa pande zote, hivyo wajumbe walikuwa wanapitia kwa umakini maelezo ya pande husika ili kufikia maamuzi sahihi.
Mgombea Michael Wambura alikata rufani kupinga kuondolewa katika mchakato wa uchaguzi wa Simba na kamati ya uchaguzi inayoongozwa na wakili, Dkt. Damas Daniel Ndumbaro.
Sababu kubwa zilizokatiwa rufani kupinga Wambura kugombea katika uchaguzi wa Simba  ni mbili ambazo ni kuipeleka Simba mahakamani  na kusimamishwa uanachama.
Taarifa za chini ya kapeti zimeshatoka, lakini si misingi yetu ya kufanya kazi kwa kuandika taarifa zisizo rasmi.
Tusubiri mkutano wa kesho baina ya mwenyekiti wa kamati ya Rufani na waandishi wa habari, hivyo wadau kuweni na subiri wakati huu ambao mnataka taarifa juu ya suala.
Mbivu na mbichi zitafahamika kama kamati ya Ndumbaro itashinda au Michael Richard Wambura.
Chukueni tahadhari juu ya taarifa zinazoendelea kutolewa na mitandao mbalimbali ya kijamii juu ya Wambura kushinda au kushindwa, jibu rasmi kutoka kwa wahusika halijatoka mpaka kesho mchana.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video