Thursday, May 8, 2014



 
ZINEDINE Zidane amekanusha tetesi kuwa anataka kuondoka Real Madrid mwishoni mwa msimu huu kwa lengo la kuanza kazi yake ya kwanza akiwa kocha mkuu.
Nyota huyo wa zamani wa Ufaransa kwasasa ni msaidizi wa Carlo Ancelotti, Santiago Bernabeu baada ya kucheza kwa mafanikio makubwa na kushinda kombe la dunia, kombe la ulaya, UEFA na makombe mawili ya ligi akiwa kwao ufaransa na Hispania.
Zidane amekuwa akihusishwa sana kurudi nyumbani kwao wiki za karibuni, huku klabu zake za zamani za Monaco na Bordeaux  zikionesha nia ya kumpatia kazi.
Zidane mwenye miaka 41 kwasasa amesisitiza kuwa hana mawasiliano yoyote na klabu hizo mbili.
“Kama kawaida, kila mtu anazungumza yake,” Zidane amewaambia L`Equipe. “na siku zote nalazimishwa kujibu hili”.
“Sina mawasiliano, hata ya siri na Monako kama ninavyosikia. Kwa kifupi, sijawahi kuwasiliana na mtu yeyote”.
“Nipo chini ya mkataba na Real Madrid, niko na Real na macho yangu yapo kwa Real, naangalia ligi kuu na ligi ya mabinngwa. Nukta!”.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video