LEJENDARI wa Ufaransa, Zinedine Zidane anaamini timu ya taifa ya nchi hiyo itafanya maajabu katika fainali za mwaka huu za kombe la dunia nchini Brazil kuanzia juni 12 hadi juni 13.
Kikosi cha kocha Didier Deschamps kwa asilimia
zote kilishindwa kufuzu fainali za kombe la dunia, lakini kilifanya maajabu
katika mechi mbili za mtoano dhidi ya Ukraine.
Zidane anaamini Karim Benzema na Frank Ribery ni
wachezaji watakaoisaidia Ufaransa kutafuta ubingwa.
“Ufaransa itafanya vizuri, “ kocha huyo msaidizi
wa Real Madrid amewaambia The times of
India.
“Mara ya mwisho nchini Afrika kusini walimvunja
moyo kila mtu, lakini kwasasa chini ya Didier Deschamps wanacheza vizuri”.
Ufaransa inaokana kuwa na nafasi ya kufuzu hatua
ya makunndi ya kombe la dunia baada ya kupangwa na nchi zinazoonekana dhaifu
ambazo ni Switzerland, Ecuador na Honduras.
Hata hivyo Zidane amewaonya wacheza wa Ufaransa
kutodharau mechi za mwanzoni kwani
wanaweza kujikuta wanapanda ndege mapema.
Aliendelea: “ uko pale kwasababu ni miongoni mwa
nchi 32 bora kwa soka duniani”.
“Katika kundi E hakuna timu yoyote inayotoka Ulaya
ukiitoa Ufaransa. Kwa asilimia kubwa hawajui mpira wetu na watacheza kwa staili
ya bara lao. Sio kundi rahisi hata kidogo”.
Wachambuzi wengi wa soka wanawapa nafasi Brazil na
Argentina kutwaa kombe la mwaka huu kutokana na kuchezwa katika ardhi yao
ambayo hakuna taifa la Ulaya lililowahi kubeba kombe.
Lakini Zidane amekataa mawazo hayo na kuamini kuwa
Ufaransa, Ujerumani na Hispania ni nchi zinazoweza kutwaa ubingwa mwaka huu.
0 comments:
Post a Comment