
Na Baraka Mpenja, Dar es salaam
MABINGWA wa soka Tanzania bara, Azam fc wamezidi
kuonesha weledi mkubwa katika uendeshaji wa klabu yao.
Ni ngumu kuwaelewa Azam jinsi wanavyofanya maamuzi
juu ya mambo yao ya msingi kuhusu klabu
na wachezaji wao.
Kwasababu watanzania wengi wanasumbuliwa na unazi
wa Simba na Yanga, ni ngumu sana kuelewa kirahisi unapotaka kuzungumza suala
kama hili.
Tangu imeingia katika soka la ushindani msimu wa
2008/2009, wachezaji wengi wa Kitanzania
na kigeni wamepita Azam.
Lakini somo kubwa la kujifunza ni namna
wanavyoondoka katika klabu hii.
Tunashuhudia katika soka la ulaya, timu zikiwa na
mawasiliano ya mapema na wachezaji
wanaotaka kuwaondoa klabuni.
Inatakumika busara kubwa kuzunguza na wachezaji
wasiowahitaji na kuwapa taarifa za mapema ili wahangaikie maisha mengine kama
wanaona bado wana uwezo wa kucheza.
Ashley Cole wa Chelsea anamaliza mkataba wake
mwishoni mwa msimu huu, na siku ya jumapili katika mchezo wa klabu yake na
Nowrich alipewa heshima kubwa baada ya mechi.
Sababu ya mashabiki na viongozi wa Chelsea kumpatia heshima hiyo ni utumishi
uliotukuka katika klabu hiyo kwa kipindi cha miaka mingi.
Lakini kitu cha msingi, Cole alishaambiwa mapema
kuwa hataongezewa mkataba, na ndio maana alimwaga machozi jumapili wakati
akiwaaga mashabiki.

Mfano wa Cole hautoshi, ipo mingi ambayo watu wote
wanaopenda mpira wanajua na hakuna haja ya kuitaja kwa leo.
Lakini Ulaya nako kuna matatizo yake juu ya kuwaacha
wachezaji hasa wa rangi nyeusi.
Wazungu kwa hili hawawezi kukwepa lawama. Kuna
wakati wanafanya maamuzi mabaya sana kwa wachezaji wa Kiafrika.
Wengi wanaamini kuwa ni ubaguzi wa rangi,
yawezekana ndiyo.
Kumbuka suala la Didier Drogba akiwa Chelsea, Yaya
Toure na Samuel Eto`o wakiwa Barcelona.
Wachezaji hawa wa Kiafrika walizifanyia kazi kubwa
mno klabu zao na kuelekea kuvunja rekodi za wazungu, lakini jinsi walivyoachwa
kwa dharau pengine wangekuwa weupe mambo yasingekuwa hivyo.
Samir Nasir, kiungo wa Manchester na timu ya taifa
ya ufaransa, kuna wakati aliwahi kukariririwa na vyombo vya habari kuwa kama
Yoya Toure angekuwa mzungu basi angekuwa akitajwa kuwa kiungo bora zaidi wa
ukabaji duniani.
Nasri alimaanisha rangi ya yaya Toure inamfanya
asipewe heshima hiyo na watu wa rangi nyeupe.
Tuachane na
hayo, yapo mengi ya kusema juu ya namna ya kuacha wachezaji katika klabu.
Lakini ulaya kwa asilimia nyingi wana weledi, japokuwa kuna changamoto kama nilivyosema
hapo juu.
Tukirudi nyumbani Tanzania, jana uongozi wa klabu ya Azam FC umefikia makubaliano ya
kuvunja Mkataba na mshambuliaji wake kutoka Ivory Coast, Ismail Kone ambaye
alikuwa anamaliza Novemba mwaka huu.
Moja ya vitu vya msingi kuvieleza katika maamuzi
hayo ni kama yafuatayo;

Mosi; namna Azam walivyozungumza na mchezaji wao
kwa kumweleza ukweli na hatimaye kufikia makubaliano ya kuvunja mkataba.
Kone ni raia wa Ivory Coast ambaye alisajiliwa kwa
malengo makubwa na Azam, lakini imekuwa tofauti na matarajio ya klabu.
Klabu imeona haihitaji huduma yake, si kwa maana
ya kushuka kiwango, hapana!, bali ni kutofiti katika mfumo wa klabu kwa sasa.
Ilielezwa kuwa Pande zote mbili zimefikia
makubaliano na mchezaji huyo amepewa haki zake na kurejea nchini mwao.
Angalia jambo hili, Kone anaitwa na uongozi wa Azam fc na kuelezwa wazi kuwa klabu haina
mpango naye, wanajadili kwa pamoja na kukubaliana kauvunja mkataba kwa njia ya
amani.
Kizuri zaidi haki zake zote anapewa na kuaga.
Sidhani kama Kone akienda kwao ataizungumza vibaya Azam fc kwasababu
wamemheshimu kwa kiwango cha juu.
Zimezoeleka sinema kwa klabu za Simba na Yanga.
Unajua ni wachezaji wangapi wanazidai klabu hizi?
Unajua kwanini TFF walikuwa wanakata mapato ya
Yanga mechi za mwishoni mwa msimu?
Unakumbaka sakata la akina John Njoroge, Wisdom
Ndlovu, Steven Malashi, juzi juzi akina Mwasyika, Nsajigwa na wengineo.
Ipo mifano mingi sana. Hata Simba nao ni hatari
sana, wapo wachezaji wengi wanaodai chao na hawajalipwa mpaka leo.
Nadhani kutolipwa haki zao kunatokana na weledi
mdogo wa wachezaji wa kitanzania kujua namna ya kudai chao.
Lakini kwa wale wanaotokea nje ya nchi wamekuwa
wakiwahenyesha sana viongozi wa Simba na Yanga.
Kwa miaka mingi, Simba na Yanga wanavunja vibaya
mikataba na wachezaji wao na kutowatendea haki hata kidogo.
Hii inatokana na kukosekana kwa weledi kwasababu
kuvunja mkataba na mtu sio vita.
Watoto wao Azam fc wanaelekea sehemu nzuri sasa.
Watu watanuna kwa hili, lakini ukweli uko hivyo. Usinune kwasababu tu unapenda
Yanga na Simba, hivyo ukiona hoja kama hii inahisi kuna unazi kwa mwandishi.
Cha msingi inapotokea mambo ya weledi mkubwa namna
hii kwa Azam fc, lazima tuikubali changamoto hii.
Pili; Azam
FC imewashukuru kwa mchango wao wachezaji wake wanne, Jabir Aziz, Ibrahim
Mwaipopo, Malika Ndeule na Omar Mtaki kwa kipindi chao chote walichoitumikia
klabu hiyo.
Wanne hao wamemaliza mikataba yao na hawataongezewa- klabu inawashukuru kwa mchango wao kwa kipindi chote tangu wajiunge nayo.
Wanne hao wamemaliza mikataba yao na hawataongezewa- klabu inawashukuru kwa mchango wao kwa kipindi chote tangu wajiunge nayo.
Azam FC pia imepokea na kuyakubali maombi ya
wachezaji wake wawili, Samih Haji Nuhu na Luckson Kakolaki kustaafu kwa sababu
mbalimbali.
Nuhu anasumbuliwa na maumivu ya goti ambalo hana matumaini ya kupona karibuni, wakati Kakolaki ameamua kustaafu ili achukue mafunzo ya ukocha.
Nuhu anasumbuliwa na maumivu ya goti ambalo hana matumaini ya kupona karibuni, wakati Kakolaki ameamua kustaafu ili achukue mafunzo ya ukocha.
Klabu imempa ajira ya kudumu Nuhu katika moja ya
viwanda vyake, wakati Kakolaki ameingizwa kwenye benchi la Ufundi la akademi ya
klabu.
Kama umesoma vizuri aya za hapo juu, utakuwa
umejifunza kitu kikubwa mno kutoka kwa Azam fc.
Cha kwanza ni kujua kutoa shukurani kwa wachezaji waliofanya
kazi katika klabu, lakini utumishi wao umefika kikomo na klabu haina mpango wa
kuendelea nao.
Hakuna kitu kizuri kama mtu kuheshimu mchango
wako. Hata katika maisha ya kawaida, unapopewa asante kwa jambo ulilofanya, huwa
inatia moyo.
Kuachana na mchezaji sio ugomvi, lazima umheshimu
na kuongea naye kwa busara.
Japokuwa hawaongezewi mikataba, lakini nadhani
hawana chuki kabisa kwasababu kwanza wamejua mapema na usajili bado kuanza,
hivyo wanao uwezo wa kutafuta kazi sehemu nyingine.
Mara ngapi wachezaji wanaachwa dakika za mwisho za
usajili katika klabu kongwe za Simba na Yanga”
Unategemea watajipanga muda gani” madhara yake
wanaweza kukosa msimu unaofuata.
Pia angalia Azam walivyomfanyia kitu kikubwa beki
wake Samih Haji Nuhu.
Majeruhi ya goti yamemfanya astaafu soka. Azam
wamemhangaikia sana mpaka kwenda naye Afrika kusini kumfanyia upasuaji.
Lengo lilikuwa ni kumrudisha uwanjani mapema,
lakini jitihada zimegonga mwamba.
Baada ya hapo Uongozi ukaona umpe ajira ya kudumu kwenye
moja ya kiwanda cha Azam. Hivi unaelewa kitu gani hapa?, ni kujua namna ya
kutoa fadhila.
Wachezaji wangapi wa Simba na Yanga wamepotea
baada ya kupata majeruhi?.
Kiggi Makasi, Victor Costa, Stephano Mwasyika…………………….ni
wengi sana na mnawajua. Wako wapi na waliachajwe na klabu zao na jitihada gani
zilifanyika kuwatibu.
Unaweza kusema mbona wengine walipelekwa India,
nenda kazungumze nao wakueleze ukweli.
Nimefanya mahojiano na wengi wao jinsi klabu zilivyowafanyia
huko India, ni aibu kubwa sana na ukitaka nitakupa ushahidi huo.
Lakini kwa Nuhu maisha mengine yataendelea
kwasababu ya kuheshimiwa na kupewa ajira baada ya viongozi kujua haweza kurudi
uwanjani mapema.
Siku ya mechi ya Taifa stars dhidi ya Burundi,
Azam walimleta Nuhu uwanja wa Taifa akiwa katika baiskeli yake ili aitazame
mechi hiyo.

Hili lilikuwa jambo zuri sana, hivi Kiggi Makasi
aliletwa na Simba? Nini hatima yake katika klabu hiyo? Najua hayupo kwenye
mipango ya kocha, lakini nini klabu yake imemfanyia? Hatufahamu.
Unakumbuka alichofanyiwa Ibrahim Shikanda baada ya
kustaafu soka Azam fc?, na sasa Kakolaki.
Wamebakishwa kuwa moja ya sehemu ya benchi la
ufundi?. Si unaoa Giggs Man United?, hata Azam mambo haya yapo kwasasa.
Kwa wakongwe wetu wachezaji wangapi walifanya
mambo makubwa na wakaachwa vibaya baada ya kumaliza kazi.
Wachache walirudi kufanya kazi baada ya
kujisomesha wenyewe.
Utataja Mkwasa, Minziro, Kibadeni, na wengine,
lakini uliza katika kusoma kwao walisaidiwa na klabu?
Wengi walijifanyiwa mambo yao na baadaye klabu
zikaona wanaweza kuzisaidia timu na ndio maana wakaingizwa benchi la ufundi,
lakini kutimuliwa imekuwa ni sehemu yao.
Sina tatizo kutimua makocha kwasababu ni utaratibu
wa dunia nzima.
Kwa haya myafanyayo Azam fc, kuna funzo kubwa kwa
Simba na Yanga.
Lengo la kutaja Simba na Yanga ni kwasababu ndizo
klabu kubwa zaidi nchini.
Kila la heri Azam fc katika harakati zenu za
kutuletea vitu vipya katika soka letu.
0 comments:
Post a Comment