Tuesday, May 6, 2014

http://2.bp.blogspot.com/-F22IsqR6gos/U10tCsUaj2I/AAAAAAAA-B0/_9xLhotqo3E/s1600/d1.jpg
Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) limeteua waamuzi kutoka Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo (DRC) kuchezesha mechi kati ya Tanzania (Ngorongoro Heroes) na Nigeria.

Mechi ya mchujo kusaka tiketi ya kucheza Fainali za 19 za Afrika kwa vijana wenye umri chini ya miaka 20 zitakazofanyika mwakani nchini Senegal itachezwa wikiendi hii jijini Dar es Salaam.

Waamuzi hao wataongozwa na Jean-Jacques Ndala Ngambo atakayesaidiwa na Oliver Safari Kabene, Nabina Blaise Sebutu na Mupemba Ignace Nkongolo. Kamishna wa mechi hiyo namba 37 ni Poiret Antoine Ralph Danny kutoka Shelisheli.

BONIFACE WAMBURA
OFISA HABARI NA MAWASILIANO
SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video