Monday, May 5, 2014



 
RUUD van Nistelrooy ameshangazwa na ofa aliyopewa na Guus Hiddink kuwa kocha wake msaidizi atakapoanza majukumu ya kukinoa  kikosi cha timu ya taifa ya Uholanzi baada ya kumalizika fainali za kombe la dunia mwaka huu nchini Brazil.
Bosi wa sasa Louis Van Gaal anatarajia kuachia nafasi hiyo baada ya kombe la dunia baadaye mwaka huu, na Hiddink anatarajiwa kurithi mikoba yake na kuiongoza Uholanzi kufuzu fainali za kombe la Ulaya mwaka 2016.
Hiddink aliyewahi kufanya kazi katika klabu za Real Madrid na Chelsea, pamoja na timu za taifa za Russia, Australia  na Korea kusini amemuomba Van Nistelrooy  kuungana naye na kuwa kocha msaidizi.
Mshambuliaji huyo wa zamani aliyefunga mabao 35 katika mechi 70 za timu yake ya taifa amekiri kuwa ofa hiyo imemshitua sana.
“Ilikuwa ni mshangao kupokea simu ya Hiddink,” ameuambia mtandao wa Uefa.com. “Kiukweli sikutegemea kitu kama kile, lakini kazi kama hii inapokuja ni heshima.
“Kufanya kazi na Hiddink mwenye uzoefu mkubwa wakati kwangu mimi ndio kwanza naanza kazi ya ukocha, ni ajabu”.
Van Nistelrooy aliongeza kuwa ana matumaini ya kusaidia soka la taifa.
“Nitakuwa kocha msaidizi, kwahiyo nitamsaidia kila mtu pamoja na kocha mwingine msaidizi Danny Blind”, Aliongeza.
“Ninaweza kutumia uzoefu wangu kuonesha namna ya kukabiliana na presha, nitaonesha namna nilivyokuwa nafanya vitu na hali iliyokuwa inanitokea-lakini ni vitu vikubwa ambavyo naweza kumfundisha kila mchezaji”.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video