Thursday, May 8, 2014



 
KOCHA wa timu ya Taifa ya Ujeruman, Joachim Law ametaja kikosi cha awali cha wanandinga 30 kwa ajili ya kombe la dunia majira ya kiangazi mwaka huu nchini Brazil, huku mshambuliaji wa Fiorentina, Mario Gomes akiachwa.
Nyota huyo wa zamani wa Bayern Municha amekuwa akisumbuliwa na majeruhi msimu huu na badala yake Low amemuita mshambuliaji kinda wa Hoffenheim, Kevin Volland.
Kipa wa Borussia Monchengladbach,  Marc-Andre ter Stegen anayehusishwa  kujiunga na Barcelona majira ya kiangazi mwaka huu naye akiachwa, huku Ron-Robert Zieler akichukuliwa kama mlinda mlango namba tatu.
Wakati huo huo, kiungo wa Real Madrid, Sami Khedira amejumuishwa katika kikosi hicho licha ya kukosa mechi nyingi kwasababu ya majeruhi.
Mbali na Volland, vijana wengi kama vile Erik Durm, Shkodran Mustafi, Matthias Ginter, Leon Goretzka na Max Meyer ni miongoni mwa wachezaji waliojumuisha katika kikosi hiki ambacho kitachujwa na kufikia wachezaji 23 ambao watatajwa juni 2 mwaka huu tayari kwa kuelekea Brazil.
Ujerumani watakutana na Ureno, Ghana na Marekani hatua ya makundi ya kombe la dunia.
KIKOSI KAMALI HIKI HAPA:
Walinda mlango : Manuel Neuer (Bayern Munich), Roman Weidenfeller (Borussia Dortmund), Ron-Robert Zieler (Hannover)    
Walinzi : Jerome Boateng (Bayern Munich), Erik Durm (Borussia Dortmund), Kevin Grosskreutz (Borussia Dortmund), Benedikt Howedes (Schalke), Mats Hummels (Borussia Dortmund), Marcell Jansen (Hamburg), Philipp Lahm (Bayern Munich), Per Mertesacker (Arsenal), Shkodran Mustafi (Sampdoria), Marcel Schmelzer (Borussia Dortmund)                     
Viungo : Lars Bender (Bayer Leverkusen), Julian Draxler (Schalke), Matthias Ginter (Freiburg), Leon Goretzka (Schalke), Mario Gotze (Bayern Munich), Andre Hahn (Augsburg), Sami Khedira (Real Madrid), Toni Kroos (Bayern Munich), Max Meyer (Schalke), Mesut Ozil (Arsenal), Bastian Schweinsteiger (Bayern Munich)    
Washambuliaji : Miroslav Klose (Lazio), Kevin Volland (Hoffenheim), Lukas Podolski (Arsenal), Marco Reus (Borussia Dortmund), Andre Schurrle (Chelsea), Thomas Muller (Bayern Munich)

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video