KIUNGO wa Barcelona, Javier Mascherano amekiri kuwa
ufalme wa klabu hiyo katika soka la Hispania na Ulaya kwa ujumla umefika
kikomo.
Wakatalunya walishindwa kutetea ubingwa wao wa La
Liga baada ya kushindwa kuwafunga Atletico Madrid kwenye uwanja wa Camp Nou
jana usiku na kumpa nafasi Diego Simeone kunyakua `ndoo`.
Atletico Madrid licha ya kuwabania Barca kutetea
taji lao, pia waliwatoa katika hatua ya robo fainali ya UEFA.
Mambo yalikuwa mabaya zaidi kwa Barca baada ya
kufungwa na Real Madrid katika fainali ya Copa del Rey na sare ya jana imewafanya
wamalize msimu bila kombe.
Mascherano anaamini kufanya vibaya msimu huu
kunadhihirisha kuwa ufalme wa Barcelona umefikia kikomo na yanatakiwa
mabadiliko makubwa, lakini alikaa kimya kuhusu hatima yake ya baadaye klabuni
hapo.
“Kuzungumzia hatima ya Mascherano ni jambo dogo
sana, kinachotakiwa ni kuizungumzia Barcelona. Ufalme umekwisha.” Aliambia Barca TV.
“klabu itafanya maamuzi na mabadiliko, lakini
lazima tukubali kuwa msimu huu haukuwa mzuri”.
Kocha Tata Martino amethibitisha kuondoka
Barcelona majira ya kiangazi mwaka huu, huku Luis Enrique akitarajiwa kurithi
mikoba yake.
0 comments:
Post a Comment