KLABU
ya Atletic Bilbao amefufua matumaini ya kucheza ligi ya mabingwa barani ulaya
msimu ujao baada ya ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Rayo Vallecano katika mchezo
wa ligi kuu nchini Hispania, La Liga usiku huu.
Bilbao chini ya kocha Ernesto Valverde wameshinda dhidi ya wenyeji wao waliopo nafasi ya katikati ya msimamo na wameongeza nguvu ya kufuzu UEFA kwa mara ya kwanza tangu walipomaliza katika nafasi ya pili katika msimu wa La Liga msimu wa 1997-98.
Wiki
iliyopita Bilbao walipata ushindi
mwingine wa mabao 3-1 dhidi ya Sevilla.
Mabao
ya kipindi cha kwanza ya Mikel San Jose dakika ya 20 na Oscar de Marcos katika
dakika ya 30 yalionesha upepo mzuri kwa Atletico Bilbao wenye `Mzuka` mkubwa wa
kuonja uhondo wa UEFA mwakani.
Mabao
hayo mawili yalisababishwa na kona mbili zilizochongwa kutoka winga ya kushoto
na mabeki wa Vallecano kushindwa kuokoa.
Baada
ya bao la De Marcos , mashabiki wa Bilbao waliingia karibu na uwanja wakiwasalimia
wachezaji na kusababisha hofu ya kukosekana kwa usalama.
Lakini
hakuna aliyepata matatizo na morali ya mashabiki wa Bilbao iliongezeka zaidi
kipindi cha pili baada ya Ander Herrera kufunga bao katika dakika ya 74 kwa
mpira wa adhabu ndogo.
Matokoe
hayo yanaifanya Bilbao kuwa mbele kwa pointi 9 dhidi ya timu ya Sevilla iliyopo
nafasi ya tano, huku ikiwa na mechi tatu, lakini haiwezi kuiondoa Bilbao katika
nafasi hiyo kutokana na kuwa dhaifu msimu huu.
0 comments:
Post a Comment