Na Baraka Mpenja
MIAMBA ya soka nchini Jamhuri ya kidemokrasia ya Kongo, TP Mazembe imepigwa kidude kimoja kwa yai dhidi ya El Hilal Omdurani ya Sudan katika mchezo wa kwanza wa hatua ya makundi ya ligi ya mabingwa barani Afrika.
MIAMBA ya soka nchini Jamhuri ya kidemokrasia ya Kongo, TP Mazembe imepigwa kidude kimoja kwa yai dhidi ya El Hilal Omdurani ya Sudan katika mchezo wa kwanza wa hatua ya makundi ya ligi ya mabingwa barani Afrika.
El Hilal walianza kutibua mipango ya Mazembe
katika dakika ya 51 baada ya Salah Al Jizoli kuandika bao la kuongoza kufuatia
kumalizia pasi nzuri ya Bakri Babeker.
Kipigo hicho cha bao 1-0 kimewafanya Mazembe
kuanza vibaya michuano hiyo na sasa watahitaji kufanya vizuri mchezoz
unaofuata, huku wakiwa katika kundi A pamoja na wapinzani wao wakubwa AS Vita.
Washambuliaji wote wawili wa Tanzania wa TPM walicheza, Mbwana Samatta akianza na Thomas Ulimwengu akitokea benchi dakika ya 66 kwenda kuchukua nafasi ya Rainford Kalaba.
Samatta na Ulimwengu wanatarajiwa kuondoka asubuhi
kuja Dar es Salaam kujiunga na timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars kwa ajili
ya mchezo wa Jumapili dhidi ya Zimbabwe, kuwania hatua ya makundi ya kuwania
tiketi ya kucheza Fainali za Mataifa ya Afrika mwakani nchini Morocc
RATIBA YA MECHI ZA KESHO NA KESHOKUTWA HII HAPA
Saturday 17 May 2014
Esperance (Tunisia) | v | ES Setif (Algeria) | 20:00 |
Sunday 18 May 2014 |
AS Vita (Congo DR) | v | Zamalek (Egypt) | 15:30 | ||
CS Sfaxien (Tunisia) | v | Al Ahly Benghazi (Libya) | 18:00 |
Saturday 24 May 2014 |
Al Ahly Benghazi (Libya) | v | Esperance (Tunisia) | 18:00 | ||
Zamalek (Egypt) | v | Al Hilal (Sudan) | 19:30 |
Sunday 25 May 2014 |
TP Mazembe (Congo DR) | v | AS Vita (Congo DR) | 15:00 | ||
ES Setif (Algeria) | v | CS Sfaxien (Tunisia) | 19:30 |
0 comments:
Post a Comment