Rais wa Shirikisho la Mpira wa
Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi amemtumia salamu za rambirambi mwenzake wa
Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo- FECOFA, Omar Constant kutokana na vifo vya
washabiki.
Washabiki 12 walipoteza maisha
uwanjani wakati wa mechi ya Ligi Kuu ya nchi hiyo kati ya TP Mazembe na AS Vita
iliyochezwa kwenye Uwanja wa Tata Raphael, jijini Kinshasa.
“Tumeguswa na msiba huo mzito, tunatoa
salamu za rambirambi kwako (Rais wa FECOFA), familia za marehemu pamoja na
wadau wote wa mpira wa miguu katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo,” imesema
sehemu ya barua hiyo ya Rais Malinzi.
0 comments:
Post a Comment