Saturday, May 3, 2014



TEGETE
Na Baraka Mpenja, Dar es salaam

MSHAMBULIAJI wa Yanga SC, Jeryson John Tegete amesema kuwa ataendelea kuitumikia klabu hiyo msimu mpya wa ligi kuu soka Tanzania bara.
Katika mahojiano maalumu na mtandao huu, Tegete ameeleza kuwa hata itokeo klabu yoyote yenye  dau nono kiasi gani hang`atuki Yanga sc.
Mshambuliaji huyo aliendelea kwa kusema Yanga ilistahili kutwaa ubingwa msimu uliopita, lakini waliathiriwa na matokeo mabaya katika mechi muhimu za mwisho, hivyo kwa nafasi yake anatarajia kuisaidia kurejesha taji msimu ujao.
“Mechi za mwisho nilipata nafasi ya kucheza na nilijisikia vizuri”.
“Muda mwingi nilikuwa sichezi na sikulalamika kwasababu nilikuwa na majeruhi ya goti”.
“Mwisho mwisho nilikuja kucheza kwasababu nilipona. Sahizi niko fiti  na msimu ujao nitacheza kwa amani sana kwasababu nimepona goti”. Alisema Tegete.
Tegete aliongeza kuwa bado ana mkataba na Yanga na hana mpango wa kuhama kwasasa kwasababu anajiona kuwa na deni kufuatia kutofanya vivuri kwa misimi miwili mitatu.
Mshambuliaji huyo kipenzi wa Wanajangwani aliendelea kueleza kuwa licha ya kuwa na deni na Yanga, bado anaota kuitumikia kwa mara nyingine  timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars.
“Taifa stars mbona nitarudi! Aaah! Nimepona goti, lazima nirudi kuonesha vitu vyangu”. Alisema Tegete kwa furaha.
Tegete pia amezungumzia kuondoka kwa wachezaji wawili wa Yanga, Frank Domayo na Didier Kavumbagu kwenda Azam fc, ambapo amekiri kuwa walikuwa muhimu, lakini hakuna haja ya kuwalilia kwasababu wapo wachezaji wengine watakaopata nafasi ya kucheza.
‘Kweli walikuwa wachezaji muhimu, lakini kuondoka kwao sio kwamba ni pengo kubwa mno”
“Wapo wachezaji wengine watakaopata nafasi. Akina Telela walikuwa hawachezi, sasa utakuwa wakati wao”.
“Mpira ndivyo ulivyo, kuondoka ni kawaida. Mashabiki wasiumize kichwa na kushindwa kulala, watu wengine wapo”.
“Mpira ni kupata nafasi ili uoneshe uwezo. Sasa wengine wakipata nafasi wataonekena”.
“Wao walipata nafasi ndio maana walionekana. Itakuwa nafasi kwa wengine pia”.
“Tusahau yaliyopita tuganye yajayo, watu wasianze kuwalaumu viongozi sana, kawaida tu”. Aliongeza Tegete.
Tegete kwa misimu miwili mfululizo ameshindwa kuonesha makali yake kama miaka ya nyuma, lakini mwishoni mwa msimu uliopita alipata nafasi ya kucheza baada ya kupona majeruhi yake ya goti.
Alifanya kazi nzuri kwa kushirikiana na Hussein Javu ambaye naye alipata nafasi mechi za mwisho.
Kwa takribani msimu mzima uliomalizika aprili 19 mwaka huu, Mrundi Didier Kavumbagu alikuwa akicheza nafasi ya mshambuliaji wa kati, lakini kwa sasa ameondoka na pengine inaweza kuwa nafasi nzuri kwa Tegete msimu ujao.

0 comments:

 
voyeur porn porn movies sex videos hd porno video